Hamia kwenye habari

Jumba la Ufalme ambapo shambulizi hilo lilitokea. Wenyeji wa Hamburg na maofisa wa serikali waliweka maua kwenye mwingilio wa Jumba ili kutoa pole

MACHI 20, 2023
UJERUMANI

Mwanamume Mmoja Awashambulia Watu Kwenye Jumba la Ufalme Jijini Hamburg, Ujerumani

Mwanamume Mmoja Awashambulia Watu Kwenye Jumba la Ufalme Jijini Hamburg, Ujerumani

Kama ilivyoripotiwa awali, Machi 9, 2023, mwanamume mmoja alishambulia kutaniko la Hamburg-Winterhude baada tu ya mikutano ya katikati ya juma kwisha. Mwanamume huyo aliwaua ndugu na dada kadhaa na kuwajeruhi wengine, na aliacha tu mashambulizi hayo maofisa wa polisi walipoingia kwenye Jumba la Ufalme, kisha akajiua. Mashahidi wa Yehova nchini Ujerumani na ulimwenguni pote wanathamini sana fadhili, upendo, na huruma ambayo wameonyeshwa na maofisa mbalimbali, mashirika, na watu kutoka sehemu mbalimbali ulimwenguni.

Athari Ambazo Ndugu na Dada Zetu Wamepata

  • Kwa kusikitisha, ndugu 4, dada 2, na mtoto ambaye hajazaliwa wa dada aliyejeruhiwa waliuawa

  • Ndugu 2 na dada 7 walijeruhiwa

Jitihada za Kutoa Msaada

  • Wawakilishi kutoka ofisi ya tawi ya Ulaya ya Kati, waangalizi wawili wa mzunguko, na wazee wa eneo hilo wanawafariji na kuwategemeza akina ndugu

Tukiwa undugu wa ulimwenguni pote wenye umoja, tunasali kwa ajili ya wote walioathiriwa na shambulizi hilo. Yehova “ni ngome katika siku ya taabu” na atatusaidia kuvumilia nyakati hizi ngumu tunapoendelea kumwabudu kwa njia yenye amani.​—Nahumu 1:7.