Hamia kwenye habari

Je, Biblia Ni Kitabu cha Wazungu?

Je, Biblia Ni Kitabu cha Wazungu?

Jibu la Biblia

 Biblia haikuandikwa na wazungu. Wanaume wote ambao Mungu alitumia kuandika Biblia walitoka Asia. Biblia haifundishi kwamba jamii moja ni bora kuliko nyingine. Hata inasema hivi: “Mungu hana ubaguzi, bali katika kila taifa mtu ambaye anamwogopa na kutenda uadilifu anakubalika kwake.”—Matendo 10:34, 35.