Hamia kwenye habari

Matatizo ya Pesa na Madeni—Je, Biblia Inaweza Kukusaidia?

Matatizo ya Pesa na Madeni—Je, Biblia Inaweza Kukusaidia?

Jibu la Biblia

 Ndiyo. Kanuni nne za Biblia zinaweza kukusaidia kutatua matatizo ya pesa na madeni.

  1.   Pangia matumizi ya pesa. “Mipango ya mwenye bidii bila shaka huleta faida, lakini kila mtu anayetenda haraka-haraka bila shaka huuelekea uhitaji.” (Methali 21:5) Usikimbilie kununua vitu kwa sababu tu vimepunguzwa bei. Panga bajeti na uifuate.

  2.   Epuka madeni yasiyo ya lazima. “Mkopaji ni mtumishi wa mtu anayemkopesha.” (Methali 22:7) Ikiwa tayari una madeni na huwezi kutimiza wajibu wako wa kulipa, jaribu kujadiliana na wakopeshaji wako na mfanye mpango mpya wa jinsi utakavyowalipa. Zungumza nao tena na tena. Fuata ushauri wa Biblia kuhusu mtu anayechukua mkopo bila kufikiri na hivyo kuwa na wajibu wa kulipa deni hilo: “Ujinyenyekeze, na sihi jirani yako; usiache macho yako kupata usingizi, wala kope zako kusinzia.” (Methali 6:1-5, Zaire Swahili Bible) Ikiwa ombi lako la kwanza litakataliwa, endelea kuwaomba wafanye marekebisho.

  3.   Uwe na maoni yanayofaa kuhusu pesa. “Mtu mchoyo ana tamaa ya kupata utajiri, naye hana habari kuwa umaskini unamngojea.” (Methali 28:22, Neno—Biblia Takatifu) Wivu na pupa zinaweza kumfilisisha mtu na pia kumfanya apuuze mambo ya kiroho.

  4.   Ridhika na vitu ulivyo navyo. “Tukiwa na chakula na kitu cha kujifunika, tutaridhika na vitu hivyo.” (1 Timotheo 6:8) Pesa haziwezi kununua furaha na uradhi. Baadhi ya watu walio na furaha nyingi ulimwenguni hawana pesa nyingi. Wanafurahia upendo wa familia na marafiki wao na ni rafiki za Mungu.​—Methali 15:17; 1 Petro 5:6, 7.