Hamia kwenye habari

Je, Mungu Ni Utatu?

Je, Mungu Ni Utatu?

Jibu la Biblia

 Dini nyingi zinazodai kuwa za Kikristo hufundisha kwamba Mungu ni Utatu. Hata hivyo ona kile ambacho Encyclopædia Britannica inasema: “Neno Utatu, wala fundisho la wazi kama hilo, halionekani katika Agano Jipya . . . Fundisho hilo lilisitawi hatua kwa hatua kwa muda wa karne kadhaa na kwa mabishano mengi.”

 Kwa kweli, Mungu wa Biblia hafafanuliwi kamwe kuwa sehemu ya Utatu. Ona mistari ifuatayo ya Biblia:

 “Yehova Mungu wetu ni Yehova mmoja.”—Kumbukumbu la Torati 6:4.

 “Wewe, ambaye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote.”—Zaburi 83:18.

 “Uzima wa milele ndio huu, waendelee kupata ujuzi juu yako wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemtuma, Yesu Kristo.”—Yohana 17:3.

 “Mungu ni mmoja tu.”—Wagalatia 3:20.

 Kwa nini dini nyingi za Kikristo husema kwamba Mungu ni Utatu?