Ayubu 33:1-33

  • Elihu amkaripia Ayubu kwa sababu ya kujiona kuwa mwadilifu (1-33)

    • Fidia yapatikana (24)

    • Kurudia nguvu za ujana (25)

33  “Lakini sasa, Ayubu, tafadhali sikiliza maneno yangu;Sikiliza kila jambo nitakalosema.   Tazama, tafadhali! Ni lazima nifumbue kinywa changu;Ni lazima ulimi wangu uzungumze.*   Maneno yangu yanatangaza unyoofu wa moyo wangu,+Na midomo yangu inasema kwa unyoofu mambo ninayojua.   Roho ya Mungu mwenyewe iliniumba,+Na pumzi ya Mweza-Yote mwenyewe ilinifanya niwe hai.+   Nijibu ikiwa unaweza;Niambie hoja zako; jitayarishe kujitetea.   Tazama! Mimi ni kama wewe mbele za Mungu wa kweli;Mimi pia niliumbwa kwa udongo.+   Kwa hiyo usiniogope,Na uzito wa maneno yangu usikulemee.   Lakini nilisikia ukisema,Naam, niliendelea kusikia maneno haya,   ‘Mimi ni safi, sina dhambi;+Mimi ni safi, sina kosa.+ 10  Lakini Mungu anatafuta sababu za kunipinga;Ananiona kuwa adui yake.+ 11  Anaitia miguu yangu katika mikatale;Anavichunguza kwa makini vijia vyangu vyote.’+ 12  Lakini umekosea kusema hivyo, kwa hiyo nitakujibu: Mungu ni mkuu sana kuliko mwanadamu anayeweza kufa.+ 13  Kwa nini unamlaumu Yeye?+ Je, ni kwa sababu hakujibu hoja zako zote?+ 14  Kwa maana Mungu huzungumza mara moja na mara ya pili,Lakini hakuna yeyote anayesikiliza, 15  Huzungumza katika ndoto, maono ya usiku,+Watu wanaposhikwa na usingizi mzitoWanapolala vitandani mwao. 16  Kisha hufungua masikio yao+Na kuyakazia* maagizo yake kwao, 17  Ili kumwepusha mtu asitende dhambi+Na kumlinda mwanadamu asiwe na kiburi.+ 18  Mungu huilinda nafsi yake isiingie* shimoni,*+Uhai wake usiangamizwe kwa upanga.* 19  Mtu hukaripiwa pia na maumivu kitandani mwakeNa mateso yasiyo na kikomo mifupani mwake, 20  Hivi kwamba nafsi yake inachukia* mkate,Naye anakataa hata chakula bora.+ 21  Nyama ya mwili wake huisha hivi kwamba haionekani,Na mifupa yake iliyokuwa imefichika sasa imechomoza.* 22  Nafsi yake inakaribia* shimoni;*Uhai wake unawakaribia wale wanaoleta kifo. 23  Ikiwa kuna mjumbe* kwa ajili yake,Mtetezi mmoja kati ya elfu moja,Ili amwambie mwanadamu mambo manyoofu, 24  Basi Mungu humhurumia na kusema,‘Mwokoe asishuke shimoni!*+Nimepata fidia!+ 25  Mwili wake na uwe na afya zaidi kuliko wakati wa ujana;+Na azirudie siku alizokuwa na nguvu za ujana.’+ 26  Atamsihi Mungu,+ naye atamkubali,Naye atauona uso wa Mungu kwa kelele za shangwe,Na Mungu atamrudishia uadilifu Wake mwanadamu anayeweza kufa. 27  Mtu huyo atawatangazia* wanadamu,‘Nimetenda dhambi+ na kupotosha yaliyo sawa,Lakini sikupokea niliyostahili.* 28  Ameikomboa nafsi yangu isiingie* shimoni,*+Na uhai wangu utaona nuru.’ 29  Kwa kweli, Mungu hufanya mambo haya yoteMara mbili, mara tatu, kwa ajili ya mwanadamu, 30  Ili kumrudisha kutoka shimoni,*Ili aweze kuangaziwa nuru ya uzima.+ 31  Sikiliza, Ayubu! Nisikilize! Nyamaza, nami nitaendelea kuzungumza. 32  Ikiwa una jambo la kusema, niambie. Sema, kwa maana nataka kuthibitisha kwamba uko sahihi. 33  Ikiwa huna la kusema, unapaswa kunisikiliza;Nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”

Maelezo ya Chini

Tnn., “Ni lazima ulimi wangu na kaakaa langu vizungumze.”
Tnn., “kuyatia muhuri.”
Au “kwa silaha.”
Au “kaburini.”
Au “huulinda uhai wake usiingie.”
Tnn., “uhai wake unachukia.”
Au “inaonekana waziwazi.”
Au “Uhai wake unakaribia.”
Au “kaburini.”
Au “malaika.”
Au “kaburini.”
Tnn., “atawaimbia.”
Au labda, “Nami sikupata faida.”
Au “Ameukomboa uhai wangu usiingie.”
Au “kaburini.”
Au “kaburini.”