Isaya 45:1-25

  • Koreshi atiwa mafuta ili aliteke Babiloni (1-8)

  • Udongo haupaswi kushindana na Mfinyanzi (9-13)

  • Mataifa mengine yatambua Israeli (14-17)

  • Mungu anategemeka katika uumbaji na katika kufunua mambo (18-25)

    • Dunia iliumbwa ili ikaliwe (18)

45  Hivi ndivyo Yehova anavyomwambia mtiwa-mafuta wake, Koreshi,+Ambaye nimeushika mkono wake wa kulia+Ili kuyatiisha mataifa mbele yake,+Kuwanyang’anya silaha* wafalme,Kufungua mbele yake milango yenye pande mbili,Hivi kwamba malango hayatafungwa:   “Mimi nitaenda mbele yako,+Nami nitavisawazisha vilima. Nitaivunja milango ya shaba vipandevipande,Nami nitayakata makomeo ya chuma.+   Nitakupa hazina zilizo gizaniNa hazina zilizofichwa mafichoni,+Ili ujue kwamba mimi ni Yehova,Mungu wa Israeli, anayekuita kwa jina lako.+   Kwa ajili ya mtumishi wangu Yakobo na Israeli niliyemchagua,Ninakuita kwa jina. Ninakupa jina la heshima, ingawa hukunijua.   Mimi ni Yehova, na hakuna mwingine yeyote. Hakuna Mungu ila mimi.+ Nitakuimarisha,* ingawa hukunijua,   Ili watu wajueKutoka mashariki hadi magharibi*Kwamba hakuna mwingine ila mimi.+ Mimi ni Yehova, na hakuna mwingine yeyote.+   Ninatengeneza nuru+ na kuumba giza,+Ninatokeza amani+ na kuumba msiba;+Mimi, Yehova, ninafanya mambo hayo yote.   Enyi mbingu, leteni mvua kutoka juu;+Mawingu na yamwage uadilifu. Dunia na ifunguke na kuzaa wokovu kwa wingi,Na ichipushe uadilifu wakati uleule.+ Mimi, Yehova, nimeiumba.”   Ole wake yule anayeshindana* na Muumba wake,*Kwa maana yeye ni kigae cha udongo tuKati ya vigae vingine vya udongo vilivyo ardhini! Je, udongo unapaswa kumuuliza Mfinyanzi:* “Unatengeneza nini?”+ Au kitu ulichokitengeneza kinapaswa kuuliza: “Yeye hana mikono”?* 10  Ole wake anayemwambia baba: “Unazaa nini?” Na kumwambia mwanamke: “Unajifungua nini?”* 11  Yehova, Mtakatifu wa Israeli na Muumba wake,+ anasema hivi: “Je, mnathubutu kuniuliza kuhusu mambo yanayokujaNa kuniamuru kuhusu wanangu+ na kuhusu kazi za mikono yangu? 12  Niliiumba dunia+ na kumuumba mwanadamu juu yake.+ Nilizitandaza mbingu kwa mikono yangu mwenyewe,+Nami ninaliamuru jeshi lake lote.”+ 13  “Nimemwinua mtu katika uadilifu,+Nami nitazinyoosha njia zake zote. Yeye ndiye atakayelijenga jiji langu+Na kuwaweka huru bila bei au rushwa+ watu wangu waliotekwa,”+ asema Yehova wa majeshi. 14  Yehova anasema hivi: “Faida ya* Misri na bidhaa za* Ethiopia na Wasabea, watu warefu,Watakuja kwako na kuwa wako. Watatembea nyuma yako wakiwa na minyororo. Watakuja na kukuinamia.+ Watasali kwako wakisema, ‘Kwa hakika Mungu yuko pamoja nawe,+Na hakuna mwingine yeyote; hakuna Mungu mwingine.’” 15  Kwa kweli wewe ni Mungu anayejificha,Ee Mungu wa Israeli, Mwokozi.+ 16  Wote wataaibishwa na kufedheheshwa;Watengenezaji wote wa sanamu wataenda zao kwa aibu.+ 17  Lakini Israeli ataokolewa na Yehova kwa wokovu wa milele.+ Hamtaaibishwa wala kufedheheshwa kwa umilele wote.+ 18  Kwa maana Yehova,Muumba wa mbingu,+ Mungu wa kweli,Yule aliyeiumba dunia, Yule aliyeitengeneza na kuifanya imara kabisa,+Ambaye hakuiumba tu bila sababu,* lakini aliiumba ili ikaliwe, anasema hivi:+ “Mimi ni Yehova, wala hakuna mwingine. 19  Sikusema nikiwa mafichoni,+ katika nchi yenye giza;Sikuuambia uzao wa* Yakobo,‘Nitafuteni tu bila sababu.’* Mimi ni Yehova, ninayesema mambo ya uadilifu na kutangaza mambo manyoofu.+ 20  Kusanyikeni pamoja mje. Karibieni pamoja, ninyi mlioponyoka kutoka kwa mataifa.+ Wale wanaobeba sanamu zilizochongwa hawajui chochoteNa wanasali kwa mungu ambaye hawezi kuwaokoa.+ 21  Toeni taarifa yenu, leteni kesi yenu. Na washauriane pamoja kwa umoja. Ni nani aliyetabiri jambo hili zamani za kaleNa kulitangaza tangu nyakati zilizopita? Je, si mimi, Yehova? Hakuna Mungu mwingine ila mimi;Mungu mwadilifu na Mwokozi,+ hakuna mwingine isipokuwa mimi.+ 22  Geukeni mje kwangu mwokolewe,+ miisho yote ya dunia,Kwa maana mimi ni Mungu, na hakuna mwingine.+ 23  Nimeapa kwa nafsi yangu;Neno limetoka kinywani mwangu katika uadilifu,Nalo halitarudi:+ Kila goti litapigwa mbele zangu,Kila ulimi utaapa kuwa mshikamanifu+ 24  Na useme, ‘Kwa hakika katika Yehova kuna uadilifu wa kweli na nguvu. Wale wote wenye ghadhabu dhidi yake watakuja mbele zake kwa aibu. 25  Katika Yehova uzao* wote wa Israeli utathibitika kuwa sawa,+Nao watajigamba katika yeye.’”

Maelezo ya Chini

Tnn., “Kuvifungua viuno vya.”
Tnn., “Nitakufunga kiuno kwa nguvu.”
Au “Kutoka mawio hadi machweo.”
Au “anayebishana.”
Au “na yule aliyemtengeneza.”
Au “yule aliyeutengeneza.”
Au labda, “Je, udongo unapaswa kusema: ‘Kazi yako haina vishikio’?”
Au “Una uchungu wa kuzaa nini?”
Au labda, “Wafanyakazi wa.”
Au labda, “wafanyabiashara wa.”
Au labda, “ili iwe tupu.”
Tnn., “Sikuiambia mbegu ya.”
Au “Nitafuteni bure.”
Tnn., “mbegu.”