Methali 3:1-35

  • Uwe na hekima na umtumaini Yehova (1-12)

    • Mheshimu Yehova kwa vitu vyenye thamani (9)

  • Hekima huleta furaha (13-18)

  • Hekima huleta usalama (19-26)

  • Mambo mema ya kuwatendea wengine (27-35)

    • Watendee wengine mema inapowezekana (27)

3  Mwanangu, usisahau mafundisho* yangu,Na moyo wako ushike amri zangu,   Kwa sababu zitakuongezea siku nyingiNa miaka ya uhai na amani.+   Usiruhusu upendo mshikamanifu na uaminifu* zikuache.+ Zifunge shingoni mwako;Ziandike kwenye kibao cha moyo wako;+   Ndipo utakapopata kibali na ufahamu mzuriMachoni pa Mungu na wanadamu.+   Mtumaini Yehova+ kwa moyo wako wote,Wala usitegemee* uelewaji wako mwenyewe.+   Katika njia zako zote mtambue yeye,+Naye atavinyoosha vijia vyako.+   Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe.+ Mwogope Yehova na ujiepushe na uovu.   Hilo litaponya mwili wako*Na kuiburudisha mifupa yako.   Mheshimu Yehova kwa vitu vyako vyenye thamani,+Kwa mavuno ya kwanza ya* mazao* yako yote;+ 10  Ndipo maghala yako yatakapojazwa kabisa,+Na mitungi yako itafurika* divai mpya. 11  Mwanangu, usikatae nidhamu ya Yehova,+Wala usichukie karipio lake,+ 12  Kwa maana Yehova huwakaripia wale anaowapenda,+Kama baba anavyomkaripia mwana anayempenda.+ 13  Mwenye furaha ni mtu anayepata hekima+Na mtu anayepata utambuzi; 14  Kupata hekima ni bora kuliko kupata fedha,Na kuipata kama faida ni bora kuliko kupata dhahabu.+ 15  Ni yenye thamani kuliko marijani;*Hakuna chochote unachotamani kinachoweza kulinganishwa nayo. 16  Maisha marefu yako katika mkono wake wa kulia;Na katika mkono wake wa kushoto kuna utajiri na utukufu. 17  Njia zake zinapendeza,Na vijia vyake vyote vina amani.+ 18  Ni mti wa uzima kwa wale wanaoishika,Na wale wanaoishika kwa nguvu wataitwa wenye furaha.+ 19  Yehova aliuweka msingi wa dunia kwa hekima.+ Aliziimarisha kabisa mbingu kwa utambuzi.+ 20  Kwa ujuzi wake vilindi vya maji vilitenganishwaNa anga zenye mawingu zilidondosha umande.+ 21  Mwanangu, zisiondoke machoni pako.* Ilinde hekima inayotumika na uwezo wa kufikiri; 22  Zitakupa uzimaNa kuwa pambo shingoni mwako; 23  Ndipo utakapotembea kwa usalama katika njia yako,Na mguu wako hautajikwaa kamwe.*+ 24  Unapolala, hutaogopa;+Utalala, na usingizi wako utakuwa mtamu.+ 25  Hutaogopa tisho lolote la ghafla+Wala dhoruba inayowajia waovu.+ 26  Kwa maana Yehova atathibitika kuwa chanzo cha uhakika wako;+Ataulinda mguu wako usinaswe.+ 27  Usiwanyime mema wale unaopaswa kuwatendea mema*+Ikiwa una uwezo wa kuwasaidia.*+ 28  Usimwambie jirani yako, “Nenda; rudi baadaye! Nitakupa kesho,” Ikiwa unaweza kumpa kitu hicho sasa. 29  Usipange kumdhuru jirani yako+Anayejihisi akiwa salama mkiwa pamoja. 30  Usigombane na mtu bila sababu+Ikiwa hajakutendea jambo lolote baya.+ 31  Usimwonee wivu mtu mkatili+Wala kuchagua yoyote kati ya njia zake, 32  Kwa maana Yehova humchukia mtu mwenye hila,+Lakini ana urafiki wa karibu na watu wanyoofu.+ 33  Laana ya Yehova iko juu ya nyumba ya mwovu,+Lakini huyabariki makao ya mwadilifu.+ 34  Kwa maana yeye huwadhihaki wale wanaodhihaki,+Lakini huwaonyesha kibali wapole.+ 35  Wenye hekima watarithi heshima,Lakini wapumbavu hutukuza aibu.+

Maelezo ya Chini

Au “sheria.”
Au “ukweli.”
Tnn., “usiegemee.”
Tnn., “kitovu chako.”
Au “mapato.”
Au “vitu vilivyo bora vya.”
Au “mashinikizo yako ya divai yatafurika.”
Angalia Kamusi.
Ni wazi kwamba mstari huu unarejelea sifa za Mungu zinazotajwa katika mistari iliyotangulia.
Au “hautagonga kamwe kitu chochote.”
Au “Ikiwa mkono wako una nguvu za kusaidia.”
Au “wale wanaostahili.”