Kwa Wafilipi 3:1-21

  • Uhakika usitegemee mwili (1-11)

    • Mambo yote ni hasara kwa ajili ya Kristo (7-9)

  • Kujinyoosha mbele kuelekea mradi (12-21)

    • Uraia mbinguni (20)

3  Mwishowe, ndugu zangu, endeleeni kushangilia katika Bwana.+ Sioni vibaya kuendelea kuwaandikia mambo yaleyale, na ni kwa ajili ya usalama wenu.  Jihadharini na mbwa; jihadharini na wale wanaosababisha madhara; jihadharini na wale wanaoukata mwili.+  Kwa maana sisi ndio wenye tohara ya kweli,+ sisi tunaotoa utumishi mtakatifu kupitia roho ya Mungu na tunaojisifu katika Kristo Yesu+ na ambao uhakika wetu hautegemei mwili,  ingawa mimi kati ya watu wote, nina sababu za kuwa na uhakika katika mwili. Mtu yeyote akifikiri ana sababu za kuwa na uhakika katika mwili, mimi ninazo zaidi:  nilitahiriwa siku ya nane,+ mimi ni wa taifa la Israeli, wa kabila la Benjamini, Mwebrania aliyezaliwa kwa Waebrania;+ kuhusu sheria, Farisayo;+  kuhusu bidii, nililitesa kutaniko;+ kuhusu uadilifu unaotegemea sheria, mtu ambaye hakuwa na hatia.  Lakini vitu vilivyokuwa faida kwangu, nimeviona kuwa hasara* kwa sababu ya Kristo.+  Isitoshe, kwa kweli ninaviona vitu vyote kuwa hasara kwa sababu ya thamani bora zaidi ya kumjua Kristo Yesu Bwana wangu. Kwa ajili yake nimekubali hasara ya vitu vyote nami ninaviona kuwa takataka nyingi, ili niweze kumpata Kristo  nami nipatikane katika muungano naye, si kwa sababu ya uadilifu wangu mwenyewe, kwa kufuata Sheria, bali kwa sababu ya uadilifu kupitia imani+ katika Kristo,+ uadilifu unaotoka kwa Mungu na unaotegemea imani.+ 10  Lengo langu ni kumjua yeye na nguvu za ufufuo wake+ na kushiriki katika mateso yake,+ nikijitiisha kwenye kifo kama chake,+ 11  ili kuona kama ikiwezekana nitaufikia ufufuo wa mapema kutoka kwa wafu.+ 12  Si kwamba tayari nimelipokea au tayari nimefanywa kuwa mkamilifu, bali ninaendelea kujitahidi+ ili kuona kama pia ninaweza kulishika lile ambalo lilifanya Kristo Yesu anichague.*+ 13  Akina ndugu, sijioni kuwa tayari nimelishika hilo; lakini jambo moja ni hakika: Ninayasahau mambo ya nyuma+ na kujinyoosha kuelekea mambo yaliyo mbele,+ 14  ninaendelea kujitahidi kuelekea mradi* kwa ajili ya tuzo+ ya mwito wa Mungu wa kwenda juu+ kupitia Kristo Yesu. 15  Kwa hiyo, wale walio wakomavu kati yetu+ na wawe na mtazamo huu wa akili, na ikiwa mna mwelekeo wa akili ulio tofauti kwa njia yoyote, Mungu atawafunulia mtazamo ulio hapo juu. 16  Kwa vyovyote, kwa kadiri ambavyo tumefanya maendeleo, na tuendelee kutembea kwa utaratibu katika mwendo huohuo. 17  Kwa muungano, iweni waigaji wangu,+ akina ndugu, na mwendelee kuwaangalia wale wanaotembea katika njia inayopatana na mfano tuliowawekea. 18  Kwa maana kuna wengi—nilikuwa nikiwataja mara nyingi lakini sasa ninawataja pia nikilia—wanaotembea kama adui za mti wa mateso* wa Kristo. 19  Mwisho wao ni uharibifu, na mungu wao ni tumbo lao, na utukufu wao kwa kweli ni aibu yao, na akili zao zinafikiria vitu vya duniani.+ 20  Lakini uraia wetu+ uko mbinguni,+ nasi tunamsubiri kwa hamu mwokozi kutoka huko, Bwana Yesu Kristo,+ 21  ambaye ataugeuza mwili wetu wa hali ya chini uwe kama* mwili wake wenye utukufu+ kwa nguvu zake nyingi zinazomwezesha kuvitiisha vitu vyote kwake mwenyewe.+

Maelezo ya Chini

Au labda, “nimeviacha kwa hiari.”
Tnn., “ambalo aliliweka juu yangu.”
Au “lengo.”
Angalia Kamusi.
Tnn., “ufanane na.”