Barua kwa Wakolosai 3:1-25

  • Utu wa zamani na utu mpya (1-17)

    • Viueni viungo vya mwili wenu (5)

    • Upendo, kifungo kikamilifu cha muungano (14)

  • Ushauri kwa familia za Kikristo (18-25)

3  Hata hivyo, ikiwa mlifufuliwa pamoja na Kristo,+ endeleeni kutafuta mambo yaliyo juu, ambako Kristo ameketi kwenye mkono wa kuume wa Mungu.+  Endeleeni kukaza akili zenu kwenye mambo yaliyo juu,+ si kwenye mambo yaliyo duniani.+  Kwa maana mlikufa, na uhai wenu umefichwa pamoja na Kristo katika muungano na Mungu.  Wakati Kristo, aliye uhai wetu,+ atakapofunuliwa, ndipo ninyi pia mtakapofunuliwa pamoja naye katika utukufu.+  Kwa hiyo, viueni viungo vya mwili wenu+ vilivyo duniani kuhusiana na uasherati,* uchafu, hamu isiyodhibitiwa ya ngono,+ tamaa yenye madhara, na pupa, ambayo ni ibada ya sanamu.  Kwa sababu ya mambo hayo ghadhabu ya Mungu inakuja.  Hivyo ndivyo pia ninyi mlikuwa mkijiendesha* katika maisha yenu ya zamani.*+  Lakini sasa, kwa kweli, lazima myaondoe mambo haya yote kutoka kwenu: ghadhabu, hasira, ubaya,+ matusi,+ na maneno machafu+ kutoka kinywani mwenu.  Msiambiane uwongo.+ Uvueni utu* wa zamani+ pamoja na mazoea yake, 10  na mjivike utu mpya,+ ambao kupitia ujuzi sahihi unafanywa kuwa mpya kulingana na mfano wa Yule aliyeuumba,+ 11  ambapo hakuna Mgiriki wala Myahudi, kutahiriwa wala kutotahiriwa, mgeni, Msikithe,* mtumwa, au mtu huru; bali Kristo ni kila kitu na yumo katika vitu vyote.+ 12  Basi, kama waliochaguliwa wa Mungu,+ watakatifu na wapendwa, jivikeni upendo mwororo wenye huruma,+ fadhili, unyenyekevu,*+ upole,+ na subira.+ 13  Endeleeni kuvumiliana na kusameheana kwa hiari+ hata ikiwa yeyote ana sababu ya kulalamika juu ya mwingine.+ Kama vile Yehova* alivyowasamehe kwa hiari, nanyi lazima mfanye vivyo hivyo.+ 14  Lakini zaidi ya mambo haya yote, jivikeni upendo,+ kwa maana huo ni kifungo kikamilifu cha muungano.+ 15  Pia, acheni amani ya Kristo itawale mioyoni mwenu,*+ kwa maana ninyi, mliitwa kwenye amani hiyo katika mwili mmoja. Na mjionyeshe kuwa wenye shukrani. 16  Neno la Kristo na likae ndani yenu kwa wingi katika hekima yote. Endeleeni kufundishana na kutiana moyo* kwa zaburi,+ sifa kwa Mungu, nyimbo za kiroho zinazoimbwa kwa shukrani,* mkimwimbia Yehova* mioyoni mwenu.+ 17  Jambo lolote mnalofanya kwa maneno au kwa matendo, fanyeni mambo yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kupitia kwake.+ 18  Enyi wake, jitiisheni kwa waume zenu,+ kwa kuwa inafaa katika Bwana. 19  Enyi waume, endeleeni kuwapenda wake zenu+ nanyi msiwakasirikie kwa uchungu.*+ 20  Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika kila jambo,+ kwa maana hilo humpendeza Bwana. 21  Enyi akina baba, msiwe mkiwakasirisha* watoto wenu,+ ili wasivunjike moyo.* 22  Enyi watumwa, watiini katika kila jambo wale ambao ni mabwana wenu wanadamu,*+ si wakati tu wanapowatazama, ili tu kuwapendeza wanadamu,* bali kwa unyoofu wa moyo, kwa kumwogopa Yehova.* 23  Lolote mnalofanya, lifanyeni kwa nafsi* yote kama kwa Yehova,*+ na si kwa wanadamu, 24  kwa maana mnajua kwamba mtapokea kutoka kwa Yehova* urithi kama thawabu.+ Mtumikieni Bwana, Kristo. 25  Hakika yule anayetenda kosa atapokea malipo kwa lile kosa alilotenda,+ na hakuna ubaguzi wowote.+

Maelezo ya Chini

Neno la Kigiriki porneiʹa. Angalia Kamusi.
Au “mlikuwa mkitembea.”
Au “mlipokuwa mkiishi hivyo.”
Tnn., “Mvueni mtu.”
Neno “Msikithe” lilimaanisha mtu asiye mstaarabu.
Au “unyenyekevu wa akili.”
Au “idhibiti mioyo yenu.”
Au “kuonyana.”
Au “neema.”
Au “msiwe wakali kwao.”
Au “msiwachokoze; msiwaudhi.”
Au “wasife moyo.”
Tnn., “si kwa matendo ya utumishi wa macho, kama wanaowapendeza wanadamu.”
Tnn., “kwa njia ya kimwili.”
Angalia Kamusi, “Nafsi.”