Barua ya Yakobo 3:1-18

  • Kuufuga ulimi (1-12)

    • Wengi hawapaswi kuwa walimu (1)

  • Hekima kutoka juu (13-18)

3  Ndugu zangu, si wengi kati yenu wanaopaswa kuwa walimu mkijua kwamba tutapokea hukumu nzito* zaidi.+  Kwa maana sisi sote hujikwaa* mara nyingi.+ Ikiwa yeyote hajikwai katika neno, huyo ni mtu mkamilifu, anayeweza kuuongoza kwa lijamu mwili wake wote pia.  Tunapoweka lijamu katika vinywa vya farasi ili watutii, sisi huuongoza mwili wao wote pia.  Tazameni hata meli: Ingawa ni kubwa sana nazo huendeshwa na upepo mkali, zinaongozwa na mtambo wa usukani ulio mdogo sana ili kwenda popote ambapo mtu aliye kwenye usukani anataka.  Vivyo hivyo pia, ulimi ni kiungo kidogo cha mwili na bado hujigamba sana. Tazameni jinsi moto mdogo unavyoweza kuteketeza msitu mkubwa!  Ulimi pia ni moto.+ Kati ya viungo vya mwili wetu, ulimi unawakilisha ulimwengu wa ukosefu wa uadilifu, kwa maana unautia mwili wote+ unajisi na kuwasha moto maisha yote* nao huwashwa moto na Gehena.*  Kwa maana kila aina ya mnyama wa mwituni, ndege, mnyama anayetambaa, na kiumbe wa baharini anaweza kufugwa na wamefugwa na wanadamu.  Lakini hakuna mwanadamu anayeweza kuufuga ulimi. Ulimi ni kitu kitundu chenye kudhuru, kilichojaa sumu yenye kuua.+  Kwa ulimi tunamsifu Yehova,* aliye Baba, na bado kwa ulimi tunawalaani wanadamu ambao wameumbwa “kwa mfano wa Mungu.”+ 10  Baraka na laana hutoka katika kinywa kilekile. Ndugu zangu, haifai mambo yatendeke hivyo.+ 11  Je, chemchemi inaweza kutoa katika shimo lilelile maji matamu* na pia machungu? 12  Ndugu zangu, je, mtini unaweza kuzaa zeituni au mzabibu kuzaa tini?+ Maji ya chumvi hayawezi kutokeza maji matamu.* 13  Ni nani mwenye hekima na uelewaji kati yenu? Na aonyeshe kwa mwenendo wake mzuri matendo yanayofanywa kwa upole unaotokana na hekima. 14  Lakini ikiwa mna wivu mkali+ na ugomvi*+ mioyoni mwenu, msiwe mkijigamba+ na kusema uwongo kuhusu ile kweli. 15  Hii siyo hekima inayoshuka kutoka juu; bali ni ya kidunia,+ ya kinyama, na ya roho waovu. 16  Kwa maana palipo na wivu na ugomvi,* pana machafuko pia na kila jambo baya.+ 17  Lakini hekima inayotoka juu kwanza kabisa ni safi,+ kisha yenye kufanya amani,+ yenye usawaziko,+ tayari kutii, yenye kujaa rehema na matunda mema,+ haina ubaguzi,+ na si ya kinafiki.+ 18  Zaidi ya hayo, tunda la uadilifu hupandwa katika hali zenye amani+ kwa* wale wanaofanya amani.+

Maelezo ya Chini

Au “kali.”
Au “hufanya makosa.”
Tnn., “mzunguko wa uhai (chanzo).”
Angalia Kamusi.
Au “yasiyo na chumvi.”
Au “yasiyo na chumvi.”
Au labda, “tamaa ya kupata mambo makuu.”
Au labda, “tamaa ya kupata mambo makuu.”
Au labda, “na.”