Zaburi 98:1-9

  • Yehova ni Mwokozi na Mwamuzi mwadilifu

    • Wokovu wa Yehova watangazwa (2, 3)

Muziki. 98  Mwimbieni Yehova wimbo mpya,+Kwa maana ametenda mambo yanayostaajabisha.+ Mkono wake wa kuume, mkono wake mtakatifu, umeleta wokovu.*+   Yehova ameutangaza wokovu wake;+Amefunua uadilifu wake mbele ya mataifa.+   Amekumbuka upendo wake mshikamanifu na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli.+ Miisho yote ya dunia imeona wokovu kutoka kwa* Mungu wetu.+   Mpazieni Yehova sauti ya ushindi, dunia yote. Changamkeni na kupaza sauti kwa shangwe na kuimba sifa.*+   Mwimbieni sifa* Yehova kwa kinubi,Kwa kinubi na wimbo mtamu.   Kwa tarumbeta na mlio wa pembe,+Pazeni sauti kwa ushindi mbele za Mfalme, Yehova.   Bahari na ingurume na vitu vyote vinavyoijaza,Dunia na wote wanaokaa humo.   Mito na ipige makofi;Milima na ipaze sauti pamoja kwa shangwe+   Mbele za Yehova, kwa maana anakuja* kuihukumu dunia. Ataihukumu kwa uadilifu dunia inayokaliwa+Na mataifa kwa haki.+

Maelezo ya Chini

Au “umemletea ushindi.”
Au “ushindi wa.”
Au “kupiga muziki.”
Au “Mpigieni muziki.”
Au “amekuja.”