Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Jinsi Mjusi Anavyojinatisha

Jinsi Mjusi Anavyojinatisha

Je, Ni Kazi ya Ubuni?

Jinsi Mjusi Anavyojinatisha

▪ Wanasayansi wanastaajabia uwezo wa mjusi wa kupanda sehemu zilizo laini—hata kujinatisha kwenye dari laini akining’inia chini—bila kuteleza! Mjusi huyu mdogo na mwenye kustaajabisha anawezaje kufanya hivyo?

Biblia inasema kwamba mjusi “hushika kwa mikono yake mwenyewe.” (Methali 30:28) Kwa kweli miguu ya mjusi inafanana na mikono, nayo ina uwezo mkubwa sana wa kunata kwenye sehemu laini. Kila kidole kina sehemu zilizo na maelfu ya vitu vinavyotokeza kama nywele. Kila kimoja cha vitu hivyo kina mamia ya nyuzinyuzi ndogo sana. Nguvu za uvutano kati ya molekuli (zinazoitwa nguvu za van der Waals) zinazotokezwa na nyuzinyuzi hizo zina uwezo wa kuhimili uzito wa mjusi—hata anaponing’inia chini akiwa amenata kwenye glasi!

Watafiti wanataka kutengeneza kitu kinachoweza kunata kwenye sehemu zilizo laini kama mjusi anavyojinatisha. * Kitu hicho kitakuwa na matumizi mengi, kutia ndani “matumizi mbalimbali ya kitiba,” linasema gazeti Science News, “kuanzia kutengeneza plasta inayonata kabla haijakauka mpaka kutengeneza nyuzi za kushonea wakati wa upasuaji.”

Baada ya kupitia habari hii fupi, una maoni gani? Je, uwezo wa mjusi wa kunata ulijitokeza wenyewe tu? Au ulibuniwa?

[Maelezo ya Chini]

^ fu. 5 Wanasayansi wanachunguza protini inayotokezwa na viumbe fulani wa majini wa jamii ya moluska, ambayo inawawezesha kujinatisha kwenye sehemu zisizo kavu.

[Picha katika ukurasa wa 26]

Upande wa chini wa mjusi anayeitwa “tokay”

[Picha katika ukurasa wa 26]

Nywele ndogo sana katika wayo wa mjusi

[Picha katika ukurasa wa 26]

Gecko: Breck P. Kent; close-up: © Susumu Nishinaga/Photo Researchers, Inc.