Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Jina la Kibiblia Katika Mtungi wa Kale

Jina la Kibiblia Katika Mtungi wa Kale

Hivi karibuni, watafiti walipendezwa na vipande vya mtungi wa udongo uliotengenezwa miaka 3,000 iliyopita, vilivyochimbuliwa mwaka 2012. Ni nini kilichokuwa cha pekee sana kuhusu uvumbuzi huo? Si vipande vya mtungi huo, bali maandishi yaliyokuwa juu ya vipande hivyo.

Wavumbuzi wa vitu vya kale walipounganisha vipande hivyo, walifaulu kusoma maandishi hayo ya kale ya Wakanaani. Maandishi hayo yalikuwa: “Eshba’al Ben [mwana wa] Beda’.” Hiyo ndiyo mara ya kwanza kwa wavumbuzi kupata jina hilo katika maandishi ya kale.

Kwa kweli, Eshbaali mwingine anatajwa katika Biblia, na alikuwa kati ya wana wa Mfalme Sauli. (1 Nya. 8:33; 9:39) Profesa Yosef Garfinkel, ambaye alishiriki katika uvumbuzi huo anasema hivi: “Inapendeza kuona kwamba jina Eshba’al linapatikana katika Biblia, na sasa pia kwenye rekodi za wavumbuzi, wakati wa utawala wa Mfalme Daudi pekee.” Baadhi ya watu hufikiri kwamba jina hilo lilitumiwa katika kipindi hicho pekee. Kwa mara nyingine tena, habari fulani inayopatikana katika Biblia imethibitishwa na wavumbuzi.

Katika andiko lingine la Biblia, jina Eshbaali limeandikwa kuwa Ish-boshethi, “boshethi” likichukua mahali pa “baali.” (2 Sam. 2:10) Kwa nini? Watafiti wanaeleza hivi: “Katika Samweli cha Pili watu walisita kutumia jina Eshba’al, ambalo lilifanana na jina la mungu wa dhoruba wa Wakanaani Ba’al, lakini jina halisi . . . lilihifadhiwa katika Kitabu cha Mambo ya Nyakati.”