Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Wanadamu wanateseka sana, hata hivyo, je, Mungu ndiye anayesababisha?

Biblia Inasema Nini?

Biblia Inasema Nini?

Je, Mungu husababisha kuteseka?

Ungejibuje?

  • Ndiyo

  • Hapana

  • Labda

Biblia inasema hivi

“Hasha, Mungu wa kweli asitende kwa uovu, na Mweza-Yote kutenda isivyo haki!” (Ayubu 34:10) Mungu hasababishi kamwe kuteseka na uovu tunaouona duniani.

Mambo mengine tunayojifunza katika Biblia

  • Shetani Ibilisi, “mtawala wa ulimwengu,” ndiye chanzo kikuu cha kuteseka. —Yohana 14:30.

  • Nyakati nyingine, maovu na kuteseka husababishwa na maamuzi mabaya ambayo huenda mtu akafanya.—Yakobo 1:14, 15.

Je, kuteseka kutaisha?

Baadhi ya watu husema kwamba wanadamu wanaweza kukomesha kuteseka kwa jitihada zao wenyewe, ilhali wengine hawaamini kuwa hali zilizo duniani zitabadilika. Wewe una maoni gani?

Biblia inasema

Mungu ataondoa kuteseka kote. “Kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.” —Ufunuo 21:3, 4.

Ni nini kingine tunachojifunza katika Biblia?

  • Mungu atamtumia Yesu kukomesha kuteseka kunakosababishwa na Ibilisi. —1 Yohana 3:8.

  • Watu wanaofanya mambo mema wataishi duniani milele.—Zaburi 37:9-11, 29.