Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Biblia Inasema Nini?

Biblia Inasema Nini?

Je, Mungu husikiliza sala zote?

JE, ANAJIBU SALA ZA  . . .

  • Kila mtu

  • Baadhi ya watu

  • Hamjibu yeyote

BIBLIA INASEMA HIVI

“Yehova yuko karibu na wote . . . wanaomwitia yeye katika ukweli.”—Zaburi 145:18.

MAMBO MENGINE TUNAYOJIFUNZA KATIKA BIBLIA

  • Mungu hasikilizi sala za watu wasiomtii. (Isaya 1:15) Hata hivyo, wanaweza ‘kunyoosha mambo’ kati yao na Yehova kwa kubadili njia zao.—Isaya 1:18.

  • Ili Mungu ajibu, ni lazima sala ipatane na matakwa yake yanayotajwa katika Biblia. —1 Yohana 5:14.

Je, unapaswa kusali ukiwa katika mkao fulani hususa?

BAADHI YA WATU WANAAMINI kwamba wanapaswa kupiga magoti, kuinamisha kichwa, au kuweka mikono pamoja wanaposali. Wewe una maoni gani?

BIBLIA INASEMA HIVI

Mungu alisikiliza watu waliosali wakiwa ‘wameketi,’ ‘wamesimama,’ ‘wamelala kifudifudi,’ au ‘kupiga magoti.’ (1 Mambo ya Nyakati 17:16; 2 Mambo ya Nyakati 30:27; Ezra 10:1; Matendo 9:40) Mungu hahitaji tuwe katika mkao fulani hususa tunaposali.

NI NINI KINGINE TUNACHOJIFUNZA KATIKA BIBLIA?