Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

WIMBO NA. 106

Kusitawisha Sifa ya Upendo

Kusitawisha Sifa ya Upendo

(1 Wakorintho 13:1-8)

  1. 1. Twasali kwa Yehova Mungu,

    Tusitawishe sifa zake.

    Zaidi ya yote upendo

    Unaotokana na roho.

    Vipawa vyetu vyote bure,

    Ikiwa hatuna upendo.

    Basi na tuwe na upendo;

    Na kumpendeza Yehova.

  2. 2. Upendo ni wenye fadhili.

    Huwafikiria wengine.

    Upendo hauna kinyongo,

    Bali husamehe wengine.

    Upendo hutusaidia,

    Kustahimili mambo yote.

    Huhimili mizigo yote.

    Upendo haushindwi kamwe.