Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

WIMBO NA. 2

Jina Lako Ni Yehova

Jina Lako Ni Yehova

(Zaburi 83:18)

  1. 1. Mwenye enzi kuu—

    Mungu uliye hai.

    Milele na milele​​—⁠

    Wewe ni Yehova.

    Tunajivunia,

    Kuitwa watu wako.

    Na duniani pote,

    Tunakutangaza.

    (KORASI)

    Yehova, Yehova,

    Wewe ndiye Mungu.

    Mbinguni na duniani,

    Hakuna mwingine.

    Wewe ndiye mweza yote,

    Wote watambue.

    Yehova, Yehova,

    Hakuna Mungu mwingine.

  2. 2. Unatuwezesha,

    Kufanya upendalo,

    Mapenzi yako wewe​​—⁠

    Wewe ni Yehova

    Mashahidi wako,

    Tunakuwakilisha.

    Heshima kubwa sana​​—⁠

    Kuwa watu wako.

    (KORASI)

    Yehova, Yehova,

    Wewe ndiye Mungu.

    Mbinguni na duniani,

    Hakuna mwingine.

    Wewe ndiye mweza yote,

    Wote watambue.

    Yehova, Yehova,

    Hakuna Mungu mwingine.