Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

WIMBO NA. 28

Kuwa Rafiki ya Yehova

Kuwa Rafiki ya Yehova

(Zaburi 15)

  1. 1. Nani rafikiyo?

    Akaaye kwako?

    Nani ambaye wamwamini?

    Nani akujua?

    Washikao Neno,

    Wakuaminio,

    Watenda haki na walio

    washikamanifu.

  2. 2. Nani awezaye

    kukukaribia?

    Umpendaye na ambaye

    wamjua jina?

    Wanaokusifu,

    Wanaokutii,

    Wote wa’minifu moyoni,

    Wasemao kweli.

  3. 3. Twakumiminia

    yaliyo moyoni.

    Unatuvuta, Watupenda,

    Nawe watutunza.

    Rafikizo wewe,

    tunataka tuwe.

    Wewe ni Rafiki mkuu,

    hakuna mwingine.