WIMBO NA. 48
Kutembea na Yehova Kila Siku
(Mika 6:8)
-
1. Twatembea na Yehova,
Tukiwa na unyenyekevu.
Anatuonyesha sisi
Fadhili tusizostahili!
Mungu ametupa fursa
Ya kutembea naye.
Hivyo twajiweka wakfu.
Twasimama na Yehova.
-
2. Shetani ana hasira,
Na mwisho unakaribia,
Tunapata upinzani
Uwezao kutuogofya.
Yehova anatulinda;
Tunamkaribia.
Twamtumikia Yeye.
Sikuzote tumpende.
-
3. Tunapata msaada
Kupitia Neno na roho,
Kutaniko la Kikristo,
Nazo sala asikiazo.
Tutembeapo na Mungu,
Anatutegemeza.
Tuwe washikamanifu,
Na kuwa wenye kiasi.
(Ona pia Mwa. 5:24; 6:9; 1 Fal. 2:3, 4.)