Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

WIMBO NA. 48

Kutembea na Yehova Kila Siku

Kutembea na Yehova Kila Siku

(Mika 6:8)

  1. 1. Twatembea na Yehova,

    Tukiwa na unyenyekevu.

    Anatuonyesha sisi

    Fadhili tusizostahili!

    Mungu ametupa fursa

    Ya kutembea naye.

    Hivyo twajiweka wakfu.

    Twasimama na Yehova.

  2. 2. Shetani ana hasira,

    Na mwisho unakaribia,

    Tunapata upinzani

    Uwezao kutuogofya.

    Yehova anatulinda;

    Tunamkaribia.

    Twamtumikia Yeye.

    Sikuzote tumpende.

  3. 3. Tunapata msaada

    Kupitia Neno na roho,

    Kutaniko la Kikristo,

    Nazo sala asikiazo.

    Tutembeapo na Mungu,

    Anatutegemeza.

    Tuwe washikamanifu,

    Na kuwa wenye kiasi.