WIMBO NA. 86
Lazima Tufundishwe
-
1. Njo’ni mjifunze kuhusu Yehova.
‘Njo’ni mnywe maji ya uzima.’
Mafunzo mema yake Yehova.
Wenye njaa wote watalishwa.
-
2. Na mikutano kamwe tusisahau,
Lazima tufundishwe na Mungu.
Hapa palipo roho ya Mungu,
Tunatembea katika nuru.
-
3. Nyimbo tuimbazo zatutia moyo!
Sauti tamu za ndugu zetu!
Tukutanike na watu Wake.
Sikuzote tusikosekane.
(Ona pia Ebr. 10:24, 25; Ufu. 22:17.)