Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo


Jinsi ya kunufaika zaidi na masomo haya ya Biblia

Jinsi ya kunufaika zaidi na masomo haya ya Biblia

Jifunze pamoja na mwalimu: Mwombe mtu aliyekupatia broshua hii akufundishe Biblia, au ujaze ombi kwenye tovuti yetu, jw.org/sw.

SEHEMU YA KWANZA

Soma kila fungu, kutia ndani maswali yaliyoandikwa kwa wino mzito (A) na maandiko (B) yanayokazia mambo makuu. Soma maandiko yaliyo na neno “soma.”

SEHEMU YA KATIKATI

Maneno yaliyo mwanzoni (C) katika sehemu ya Chimba Zaidi yanaeleza habari ambazo zitazungumziwa. Vichwa vidogo (D) vinaonyesha mambo makuu. Soma maandiko, jibu maswali, na utazame video (E).

Chunguza picha kwa makini na maelezo ya picha (F), na ufikirie jinsi unavyoweza kujibu swali lililo chini ya Watu Fulani Husema (G).

SEHEMU YA MWISHO

Somo linakamilishwa kwenye sehemu ya Muhtasari na Ungejibuje? (H) Andika tarehe ambayo somo limekamilishwa. Kwenye Lengo (I) kuna sehemu ya mambo ambayo unaweza kufanyia kazi. Chini ya Chunguza Zaidi (J) kuna habari za ziada ambazo unaweza kusoma au kutazama.

Jinsi ya kupata mistari ya Biblia

Maandiko yanaonyeshwa kwa kitabu cha Biblia (A), sura (B), na mstari au mistari (C). Kwa mfano, Yohana 17:3 inamaanisha kitabu cha Yohana, sura ya 17, mstari wa 3.