Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Uzee; Wenye Umri Mkubwa; Wazee

Uzee; Wenye Umri Mkubwa; Wazee

Ni nini hutokea miaka yetu inaposonga?

Zb 71:9; 90:10

Je, wazee wanaweza kudumisha shangwe yao licha ya majaribu na kutoweza kufanya mambo mengi kutokana na kusonga kwa umri?

2Ko 4:​16-18; Yak 1:​2-4

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 1Sa 12:​2, 23—Nabii Samweli aliyezeeka anajua jinsi ilivyo muhimu aendelee kusali kwa niaba ya watu wa Yehova

    • 2Sa 19:​31-39—Mfalme Daudi anathamini sana jinsi Barzilai aliyezeeka anavyomtegemeza kwa uaminifu, na Barzilai anaonyesha sifa ya kiasi kwa kutambua mambo asiyoweza kutimiza anapoombwa afanye mambo yanayopita uwezo wake

    • Zb 71:​9, 18—Mfalme Daudi anapoogopa kwamba hatatumiwa tena na Yehova kwa sababu amezeeka, anamwomba Yehova asimtupe bali ampatie nguvu ili aweze kufundisha kizazi kijacho kumhusu Yeye

    • Lu 2:​36-38—Nabii wa kike Ana, ambaye ni mjane aliyezeeka, anabarikiwa kwa sababu ya kujitoa kwa Mungu na kumtumikia kwa uaminifu

Yehova anawahakikishia jinsi gani wenye umri mkubwa kwamba anawathamini?

Zb 92:​12-14; Met 16:31; 20:29; Isa 46:4; Tit 2:​2-5

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mwa 12:​1-4—Akiwa na umri wa miaka 75, Abrahamu anapata mgawo kutoka kwa Yehova unaobadili maisha yake

    • Da 10:​11, 19; 12:13—Malaika anamtembelea nabii Danieli, ambaye ana miaka 90 hivi, ili kumhakikishia kwamba ni mwenye thamani sana kwa Yehova na kwamba atathawabishwa kwa sababu ya uaminifu wake

    • Lu 1:​5-13—Yehova anawabariki Zekaria na Elisabeti waliozeeka kwa kuwasaidia kimuujiza kupata mwana anayeitwa Yohana

    • Lu 2:​25-35—Yehova anafanya Simeoni aliyezeeka apate shangwe kwa kumruhusu amwone mtoto ambaye angekuja kuwa Masihi; Simeoni anatoa unabii ulioongozwa na roho kumhusu mtoto huyo

    • Mdo 7:​23, 30-36—Nabii Musa ana umri wa miaka 80 anapopewa mgawo na Yehova wa kuwaongoza watu Wake, Israeli

Waaminifu waliozeeka wanapaswa kutendewaje?

Law 19:32; 1Ti 5:1

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

Ni katika njia gani hususa Wakristo wanaweza kuwasaidia wenye umri mkubwa kutanikoni?