Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 1

Mashahidi wa Yehova Ni Watu wa Aina Gani?

Mashahidi wa Yehova Ni Watu wa Aina Gani?

Denmark

Taiwan

Venezuela

India

Unawajua Mashahidi wa Yehova wangapi? Baadhi yetu ni majirani, wafanyakazi, au hata wanafunzi wenzako. Huenda tumewahi kuzungumza nawe kuhusu Biblia. Sisi ni akina nani, na kwa nini tunawaeleza watu kuhusu imani yetu hadharani?

Sisi ni watu wa kawaida. Tumetoka katika malezi na jamii tofauti-tofauti. Baadhi yetu walikuwa wafuasi wa dini mbalimbali na hata wengine hawakuamini kuna Mungu. Hata hivyo, kabla ya kuwa Mashahidi, sote tulichunguza kwa makini mafundisho ya Biblia. (Matendo 17:11) Tuliamini mambo tuliyojifunza, kisha tukaamua sisi wenyewe kumwabudu Yehova Mungu.

Tunafaidika kwa kujifunza Biblia. Kama watu wengine, sisi pia tunakabiliana na matatizo na udhaifu wetu wenyewe. Lakini kwa kujitahidi kutumia kanuni za Biblia katika maisha yetu ya kila siku, tunajionea mabadiliko makubwa maishani. (Zaburi 128:1, 2) Hiyo ndiyo sababu moja inayofanya tuwaeleze wengine kuhusu mambo mazuri ambayo tumejifunza katika Biblia.

Tunaishi kulingana na viwango vya Mungu. Viwango hivyo tunavyojifunza katika Biblia vinatusaidia kuwa na hali njema na kuwaheshimu wengine, kutia ndani kuwa na sifa kama vile unyoofu na fadhili. Viwango hivyo vinatusaidia pia kuwa watu wazuri na wenye manufaa katika jamii. Isitoshe, vinasaidia familia kuwa na umoja na mwenendo mzuri. Kwa sababu tuna uhakika kwamba “Mungu hana ubaguzi,” sisi ni familia kubwa ya ulimwenguni pote ambayo haina ubaguzi wa kijamii wala wa kisiasa. Ingawa sisi ni watu wa kawaida tu, kuna tofauti kati yetu na vikundi vingine.—Matendo 4:13; 10:34, 35.

  • Ni mambo gani yanayoonyesha kwamba Mashahidi wa Yehova ni watu wa kawaida tu?

  • Mashahidi wamejifunza viwango gani katika Biblia?