Ona video zinazopatikana

Biblia Inasema Nini Kuhusu Ngono ya Wanaume kwa Wanaume ao Wanawake kwa Wanawake?

Biblia Inasema Nini Kuhusu Ngono ya Wanaume kwa Wanaume ao Wanawake kwa Wanawake?

Jibu la Biblia

 Mungu alitaka ngono ao kitendo cha ndoa kifanywe tu kati ya mwanaume na mwanamuke ambao wameoana. (Mwanzo 1:​27, 28; Walawi 18:22; Methali 5:​18, 19) Biblia inakataza ngono kati ya mwanaume na mwanamuke ambao hawajaoana, kati ya wanaume kwa wanaume, wanawake kwa wanawake. (1 Wakorintho 6:​18) Uasherati unatia ndani ngono kati ya watu ambao hawajaoana, kugusa-gusa viungo vya uzazi vya mwengine, ngono ya kinywa ao ngono ya mukundu.

 Biblia inakataza ngono kati ya wanaume na wanaume ao kati ya wanawake na wanawake, lakini hilo halimaanishe kwamba tunapaswa kuchukia wale wanaofanya matendo hayo. Tofauti na hilo, Biblia inatushauri ‘tuheshimu watu wote.’​—1 Petro 2:​17, Verbum Bible.

 Mutu anaweza kuzaliwa na tamaa hiyo chafu?

Biblia haizungumuzie waziwazi ikiwa tamaa hizo zinatoka wapi, lakini inaonyesha kwamba sisi wote tumezaliwa na tamaa ya kuasi amri za Mungu. (Waroma 7:​21-​25) Kuliko kuzungumuzia kwa urefu namna tamaa hizo zinavyoanza, Biblia inakataza ngono ya wanaume kwa wanaume ao wanawake kwa wanawake.

 Namna ya kumupendeza Mungu ijapokuwa kuwa na tamaa hizo.

Biblia inasema hivi: ‘Musiache mwili wenu uwatawale. Muue kila tamaa ya uasherati.’ (Wakolosai 3:5, Contemporary English Version) Ili kuua tamaa mbaya, ambazo zinaongoza kwenye matendo mabaya, unapaswa kulinda akili yako. Ikiwa kila mara unaingiza mawazo mazuri katika akili yako, hilo linaweza kukusaidia usiwe na tamaa mbaya. (Wafilipi 4:8; Yakobo 1:​14, 15) Inaweza kuwa vigumu sana mwanzoni, lakini inawezekana. Mungu anaahidi kukusaidia ili ‘ufanywe upya katika nguvu zinazoendesha akili yako.’​—Waefeso 4:​22-​24.

 Inaweza kuwa vigumu pia hata kwa watu wengine kujiambatanisha na kanuni za Biblia. Kwa mufano, wale ambao hawana tumaini ya kuoa ao kuolewa karibuni ao wale ambao wameolewa na mutu ambaye hawezi kufanya ngono kwa sababu ya ulemavu fulani wanajikaza kuzuia tamaa zao ijapokuwa majaribu wanayoweza kukutana nayo. Hata hivyo, wanaishi kwa furaha. Kwa hiyo wanaume ao wanawake walio na tamaa ya kufanya ngono na wanaume ao wanawake wenzao wanaweza pia kujikaza ikiwa wanataka kabisa kumupendeza Mungu.​—Kumbukumbu la Torati 30:19.