Ona video zinazopatikana

Je, Mungu Atanisaidia Ikiwa Ninasali?

Je, Mungu Atanisaidia Ikiwa Ninasali?

Jibu la Biblia

 Ndiyo, Mungu anawasaidia wale wanaomuomba kwa bidii mambo yanayopatana na mapenzi yake. Kuna watumishi wa Mungu waliosali hivi: “Ee Mungu, unisaidie.” Hata ikiwa haukuwa na zoea la kusali hapo mbele, mifano yao inaweza kukutia moyo. Ona mifano fulani.

  •   ‘Unisaidie, Ee Yehova Mungu wangu; uniokoe kulingana na fazili zako zenye upendo.’—Zaburi 109:26.

  •   “Wamenitesa bila sababu. Ee unisaidie.”—Zaburi 119:86.

 Bila shaka, yule aliyeandika maneno hayo alikuwa na imani yenye nguvu katika Mungu. Hata hivyo, Mungu anasikiliza sala za wale wote wanaomuendea wakiwa na maoni mazuri, kama vile wale “waliovunjika moyo” ao “waliopondwa roho.”—Zaburi 34:18.

 Usifikiri kwamba Mungu iko mbali sana nawe na haone matatizo yako. Biblia inasema hivi: ‘Kwa maana Yehova yuko juu, hata hivyo yeye humuona munyenyekevu; lakini yeye anamujua mwenye kiburi kutoka mbali tu.’ (Zaburi 138:6) Zaidi ya hilo, siku moja Yesu aliwaambia wanafunzi wake hivi: “Lakini nywele zenyewe za kichwa chenu zimehesabiwa zote.” (Mathayo 10:30) Ikiwa Mungu anajua habari zinazokuhusu ambazo hata wewe haujue, je, hauone kwamba iko tayari kukusikiliza ikiwa unamuomba akusaidie kupambana na matatizo yako?—1 Petro 5:7.