Ona video zinazopatikana

Mungu Njo Anatuleteaka Mateso?

Mungu Njo Anatuleteaka Mateso?

Jibu ya Biblia

 Bila kuenda huku na huku, Biblia inajibia hapana! Wakati Mungu aliumba wanadamu, hakupendaka wakuwe wanateseka. Lakini wanadamu wa kwanza walikatala kumutii Mungu, wakachagua kujiamulia mambo ya muzuri na ya mubaya. Walimuacha Mungu, na ile iliwaletea magumu.

 Leo, na siye tuko tunateseka juu ya uamuzi mubaya wenye walikamataka. Kwa hiyo, haiko Mungu njo analeteaka wanadamu mateso.

 Biblia inasema hivi: “Wakati mutu iko katika jaribu, asiseme: ‘Mungu ananijaribu.’ Kwa maana Mungu hawezi kujaribiwa na mambo maovu, wala yeye mwenyewe hamujaribu mutu yeyote.” (Yakobo 1:13) Watu wote wanaweza kuteseka, hata watu wenye kumutumikia Mungu.