Ona video zinazopatikana

Roho Takatifu Ni Nini?

Roho Takatifu Ni Nini?

Jibu ya Biblia

 Roho takatifu ni nguvu yenye Mungu anatumiaka juu ya kufanya mambo mbalimbali. (Mika 3:8; Luka 1:35) Wakati Biblia inasema kama Mungu anatuma roho yake, ile inamaanisha kama anatumia nguvu yake fasi yoyote kwenye anapenda juu ya kutimiza mapenzi yake.​—Zaburi 104:30; 139:7.

 Mu Biblia, neno “roho” inatokana na neno ya Kiebrania ruʹach na neno ya Kigiriki pneuʹma. Mara mingi, ile maneno inamaanisha roho takatifu, ni kusema, nguvu yenye Mungu anatumiaka juu ya kufanya mambo mbalimbali. (Mwanzo 1:2) Lakini, ile maneno inatumiwaka pia juu ya kumaanisha mambo yenye kufuata:

 Ile maana yote inazungumuzia kitu yenye mwanadamu hawezi kuona, lakini anaweza kuona mambo yenye ile kitu kinafanya. Vilevile, roho takatifu ya Mungu, “sawa vile tu upepo, haionekanake, na iko na nguvu.”​—An Expository Dictionary of New Testament Words, cha W. E. Vine.

 Biblia inaita roho takatifu kuwa “mikono” ao “vidole” vya Mungu. (Zaburi 8:3; 19:1; Luka11:20; linganisha na Matayo 12:28.) Sawa tu vile fundi anatumiaka mikono yake juu ya kufanya kazi yake, Mungu alitumiaka roho yake juu ya:

Roho takatifu haiko mutu

 Juu Biblia inaita roho takatitu kuwa “mikono,” “vidole,” ao “pumuzi” ya Mungu, ile inaonyesha kama roho takatifu haiko mutu. (Kutoka 15:8, 10) Mikono ya fundi haiwezi kufanya kazi bila kuongozwa na akili yake. Vilevile, roho takatifu haiwezi kufanya kazi bila kuongozwa na Mungu. (Luka 11:13) Tena, Biblia inalinganisha roho ya Mungu na maji, na inaitaya pamoja na imani na ujuzi. Ile yote inaonyesha kama roho takatifu haiko mutu.​—Isaya 44:3; Matendo 6:5; 2 Wakorinto 6:6.

 Biblia inasema kama jina ya Mungu ni Yehova, jina ya Mwana wake ni Yesu Kristo, lakini hakuna fasi kwenye inasema jina ya roho takatifu. (Isaya 42:8; Luka 1:31) Wakati walikuwa wanamuua Stefano kwa sababu ya imani yake, ule Mukristo aliona katika maono mambo yenye kuwa mbinguni. Aliona tu watu mbili, hapana watu tatu. Biblia inasema hivi: “Yeye, akiwa amejaa roho takatifu, akaangalia mbinguni na akaona utukufu wa Mungu na Yesu akiwa amesimama kwenye mukono wa kuume wa Mungu.” (Matendo 7:55) Roho takatifu njo nguvu yenye Mungu alitumiaka juu ya kusaidia Stefano aone ile maono.

Mawazo fulani yenye haiko ya kweli juu ya roho takatifu

 Watu fulani wanasemaka: Roho takatifu ni mutu na ni sehemu ya utatu, sawa vile 1 Yohana 5:7, 8 inaonyesha mu tafsiri ya Biblia yenye kuitwa Verbum Bible.

 Kweli njo hii: Mu 1 Yohana 5:7, 8, Verbum Bible inaongeza maneno “mbinguni, Baba, Neno na Roho Mtakatifu, na watatu hawa ni moja. Tena wako watatu wenye kushuhudia duniani.” Lakini, watu wenye kufanya uchunguzi wamevumbula kama ile maneno haikuandikwa na mutume Yohana na kwa hiyo haistahili kuwa mu Biblia. Bruce M. Metzger, mwalimu ku masomo ya juu, aliandika hivi: “Tuko hakika kama ile maneno haiko ya kweli na haistahili kuwa mu Agano Jipya.”​—A Textual Commentary on the Greek New Testament.

 Watu fulani wanasemaka: Wakati Biblia inazungumuzia roho takatifu, inaizungumuziaka sawa vile ni mutu. Ile inaonyesha kama roho takatifu ni mutu.

 Kweli njo hii: Wakati fulani, Biblia inazungumuziaka roho takatifu sawa vile ni mutu, lakini ile haionyeshe kama roho takatifu ni mutu. Biblia inazungumuzia pia hekima, kifo, na zambi sawa vile ni mutu. (Mezali 1:20; Waroma 5:17, 21) Kwa mufano, Biblia inaonyesha kama hekima iko na “kazi” na “watoto,” na kama zambi inakuwaka inashawishi, inaua, na kutokeza tamaa.​—Matayo 11:19; Luka 7:35; Waroma 7:8, 11.

 Kwa mufano, wakati mutume Yohana alitaya maneno ya Yesu, alizungumuzia roho takatifu sawa vile ni mutu kwa kuiita kuwa “musaidizi” (paraclet) mwenye angeweza kutoa Ushahidi, kuongoza, kuzungumuza, kusikia, kutangaza, kutukuza, na kupokea. (Yohana 16:7-​15) Lakini, ile haimaanishe kama roho takatifu ni mutu.

 Watu fulani wanasemaka: Juu Biblia inasema kama tunapaswa kubatizwa mu jina la roho takatifu, ile inaonyesha kama roho takatifu ni mutu.

 Kweli njo hii: Wakati fulani, Biblia inatumiaka neno “jina” juu ya kuzungumuzia uwezo ao mamlaka. (Kumbukumbu la Torati 18:5, 19-​22; Esta 8:10) Mutu mwenye anabatizwa katika “jina la” roho takatifu anatambua uwezo na kazi ya roho takatifu katika kutimiza mapenzi ya Mungu.​—Matayo 28:19.

 Watu fulani wanasemaka: Mitume wa Yesu na wanafunzi wengine wa kwanza-kwanza waliamini kama roho takatifu ni mutu.

 Kweli njo hii: Biblia haiseme vile, na historia haionyeshe vile. Kitabu Encyclopædia Britannica inasema hivi: “Kusema kama roho takatifu ni mutu pia mwenye anapaswa kuabudiwa . . . kulianzia ku mukutano wenye ulifanywa Constantinople mu mwaka wa 381.” Ile ilikuwa miaka zaidi ya 250 kisha kifo ya mutume wa mwisho.