Ona video zinazopatikana

Yehova Ni Nani?

Yehova Ni Nani?

Jibu ya Biblia

 Yehova njo Mungu wa kweli mwenye Biblia inazungumuzia, na yeye njo aliumba vitu vyote. (Ufunuo 4:11) Nabii Abrahamu na Musa walikuwa wanamuabudu, na Yesu naye. (Mwanzo 24:27; Kutoka 15:1, 2; Yohana 20:17) Haiko Mungu wa taifa moja tu, lakini wa “dunia yote.”​—Zaburi 47:2.

 Biblia inaonyesha kama Yehova ni jina ya pekee ya Mungu. (Kutoka 3:15; Zaburi 83:18) Inatokana na neno ya Kiebrania yenye kumaanisha “kuwa,” na watu wengi wenye elimu wanasema kama ile jina inamaanisha “Yeye Anafanya Kuwa.” Jina yenye iko na ile maana inastahili kabisa Yehova juu yeye ni Muumbaji na anatimizaka makusudi yake. (Isaya 55:10, 11) Biblia inatusaidia pia kujua sifa za mwenye ile jina, zaidi sana sifa yake kubwa ya upendo.​—Kutoka 34:5-7; Luka 6:35; 1 Yohana 4:8.

 Mu Kiebrania, jina ya Mungu ilikuwa inaandikiwa na herufi ine יהוה (YHWH), zenye zinaitwa Tetragramatoni. Mu Swahili (Congo), zile herufi zinatafsiriwa Yehova. Haijulikane namna ile jina ilikuwa inatamukwa mu Kiebrania ya zamani. Lakini jina “Yehova” imetumiwa kwa miaka mingi mu luga za mingi. Ile jina ilionekana kwa mara ya kwanza mu Kiiingereza mu tafsiri ya Biblia ya William Tyndale ya 1530. *

Juu ya nini hatujue namna jina ya Mungu ilikuwa inatamukwa mu Kiebrania ya zamani?

 Kiebrania ya zamani iliandikwa kwa kutumia tu konsone (kwa mufano b, c, d, f, . . .), haikutumia vwayele (a, e, i, o, u). Musomaji wa Kiebrania alikuwa anajitilia vwayele fasi kwenye ilikuwa inafaa. Lakini, wakati kazi ya kuandika Maandiko ya Kiebrania (“Agano ya Kale”) ilimalizika, Wayahudi fulani walianza kuamini mawazo ya ushirikina yenye kuonyesha kama ni kosa kutaya jina ya pekee ya Mungu. Wakati walisoma andiko yenye ilikuwa na jina ya Mungu, walibadilisha jina Yehova na majina kama vile “Bwana” ao “Mungu.” Kadiri miaka ilipita, ile mawazo ya ushirikina ilienea sana na watu hawakujua tena namna jina ya Mungu ilikuwa inatamukwa zamani. *

 Watu fulani wanawaza kama jina ya Mungu ilikuwa inatamukwa “Yahweh,” na wengine wanaleta mawazo ingine mbalimbali. Kitabu ya Kukunjwa ya Bahari ya Chumvi yenye iko na sehemu ya kitabu ya Mambo ya Walawi mu Kigiriki inatafsiri ile jina kuwa Iao. Waandikaji wa zamani wa Kigiriki walionyesha pia kama ile jina inaweza kutamukwa Iae, I·a·beʹ, na I·a·ou·eʹ, lakini hakuna ushuhuda wenye unaonyesha kama ni vile jina ya Mungu ilikuwa inatamukwa mu Kiebrania ya zamani. *

Mawazo fulani yenye haiko ya kweli juu ya jina ya Mungu

 Watu fulani wanasemaka: Tafsiri zenye zinatumia jina “Yehova” zimeongeza ile jina.

 Kweli njo hii: Jina ya Mungu yenye kuandikwa mu Tetragramatoni inapatikana mara 7000 hivi mu Biblia. * Tafsiri za mingi za Biblia zimetosha jina ya Mungu na pa nafasi yake zimetia majina ya cheo, sawa vile “Bwana.”

 Watu fulani wanasemaka: Mungu Mweza-Yote hana lazima ya kuwa na jina ya pekee.

 Kweli njo hii: Mungu njo aliongoza waandikaji wa Biblia watumie jina yake mara mingi sana, na anaomba wale wenye kumuabudu waitumie. (Isaya 42:8; Yoeli 2:32; Malaki 3:16; Waroma 10:13) Na hata, Mungu alilaumu manabii wa uongo wenye walijaribu kufanya watu wasahau jina yake.​—Yeremia 23:27.

 Watu fulani wanasemaka: Kulingana na mawazo ya Wayahudi, jina ya Mungu inapaswa kuondolewa mu Biblia.

 Kweli njo hii: Ni kweli kwamba waandishi fulani Wayahudi walikatala kutamuka jina ya Mungu. Lakini hawakuitosha mu kopi zao za Biblia. Mungu hapendi tufuate mawazo ya wanadamu yenye haipatane na amri zake.​—Matayo 15:1-3.

 Watu fulani wanasemaka: Jina ya Mungu haipaswe kutumiwa mu Biblia juu haijulikane kabisa ilikuwa inatamukwa namna gani mu Kiebrania.

 Kweli njo hii: Kufikiri vile ni kutafuta kuonyesha kama Mungu anaomba watu wenye wanazungumuza luga tofauti-tofauti watamuke jina yake kwa njia ileile. Lakini Biblia inaonyesha kama watumishi wa Mungu wa zamani wenye walikuwa wanazungumuza luga mbalimbali walitamuka majina ya pekee mu njia tofauti-tofauti.

 Kwa mufano, fikiria muamuzi Mwisraeli mwenye kuitwa Yoshua. Wakristo wa karne ya kwanza wenye walikuwa wanazungumuza Kiebrania wangetamuka jina yake Yehoh·shuʹaʽ, lakini wale wenye kuzungumuza Kigiriki wangemuita I·e·sousʹ. Mu Biblia muko jina ya Kigiriki ya Yoshua yenye ilitafsiriwa kutoka mu Kiebrania. Ile inaonyesha kama Wakristo walitumia majina ya pekee sawa vile tu watu walizoea kuitumia mu luga yao.​—Matendo 7:45; Waebrania 4:8.

 Ni vile pia kuhusu kutafsiri jina ya Mungu. Kuliko tu kuhangaikia namna ile jina ilikuwa inatamukwa, jambo ya maana zaidi ni kutia ile jina fasi kwenye inapaswa kuwa mu Biblia.

^ Tyndale alitumia jina “Iehouah” mu tafsiri yake ya vitabu tano vya kwanza vya Biblia. Kadiri wakati ilipita, luga ya Kiingereza iliendelea kubadilika. Kwa hiyo, jina ya Mungu ilianza kuandikwa kulingana na namna watu walikuwa wanaandika ile wakati. Kwa mufano, mu mwaka wa 1612, Henry Ainsworth alitumia jina “Iehovah” mu tafsiri yake yote ya kitabu ya Zaburi. Wakati alirekebisha ile tafsiri mu mwaka wa 1639, alitumia jina “Jehovah.” Vilevile, watafsiri wa Biblia ya American Standard Version yenye ilichapishwa mu mwaka wa 1901, walitumia jina “Jehovah” kila fasi kwenye jina ya Mungu ilipatikana mu maandishi ya Kiebrania.

^ Kitabu New Catholic Encyclopedia, Toleo ya Pili, Buku ya 14, ukurasa wa 883-​884, inasema hivi: “Wakati fulani kisha Wayahudi kutoka mu uhamisho walianza kuheshimia jina Yahweh kupita kiasi, na kwa hiyo pa nafasi yake wakaanza kutumia majina ya cheo ADONAI ao ELOHIMU.”

^ Juu ya kupata habari zaidi, ona Nyongeza A4, “Jina la Mungu Katika Maandiko ya Kiebrania,” mu Biblia​—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya.

^ Ona kitabu Theological Lexicon of the Old Testament, Buku ya 2, ukurasa wa 523-​524.