Ya Kwanza kwa Watesalonike 2:1-20

  • Utumishi wa Paulo katika Tesalonike (1-12)

  • Watesalonike walikubali neno la Mungu (13-16)

  • Paulo anatamani kuona Watesalonike (17-20)

2  Kwa kweli, ndugu, ninyi wenyewe munajua kama wakati tuliwatembelea, haikukuwa bila matokeo.+  Kwa maana hata kama tuliteseka kwanza na kutendewa kwa zarau kule Filipi,+ kama vile munajua, Mungu wetu alitufanya tusikuwe na woga* ili tuwatangazie ninyi habari njema ya Mungu+ katika upinzani mwingi.*  Kwa maana mambo yenye tunawatia moyo* kufanya hayatokane na kosa, ao uchafu, ao udanganyifu,  lakini kama vile tumekubaliwa na Mungu kuwa tunastahili kupewa kazi ya kuhubiri habari njema, basi hatuseme ili kupendeza wanadamu, lakini ili kumupendeza Mungu, mwenye anachunguza mioyo yetu.+  Kwa kweli, munajua kama hatukutumia hata siku moja maneno ya kusifu-sifu ao kujiendesha kwa unafiki kwa sababu ya pupa;+ Mungu ni shahidi!  Na hatukutafuta utukufu kutoka kwa wanadamu, ikuwe ni kutoka kwenu ao kutoka kwa watu wengine, hata kama tukiwa mitume wa Kristo, tungewawekea ninyi muzigo muzito wa kututunza.*+  Kuliko kufanya vile, tulikuwa wapole katikati yenu, kama vile wakati mama mwenye kunyonyesha anahangaikia* kwa upendo watoto wake mwenyewe.  Basi, kwa kuwa tulikuwa na upendo wenye upole* kuwaelekea ninyi, hatukupenda tu kuwapatia ninyi habari njema ya Mungu, lakini pia tulipenda kuwapatia uzima wetu* wenyewe,+ kwa sababu mulikuwa wapendwa sana kwetu.+  Hakika ndugu, munakumbuka kazi yetu ya jasho na kazi yetu ya taabu. Tulikuwa tunatumika usiku na muchana, ili tusiweke muzigo muzito juu ya mutu yeyote kati yenu,+ wakati tuliwahubiria ninyi habari njema ya Mungu. 10  Ninyi ni mashahidi, na Mungu pia, juu ya namna tulijiendesha kwenu ninyi waamini kwa ushikamanifu na kwa haki na bila lawama. 11  Munajua muzuri kama tuliendelea kutia moyo,* kufariji, na kumutolea ushahidi kila mumoja wenu,+ kama vile baba+ anatendea watoto wake, 12  ili muendelee kutembea kwa namna yenye kumustahili Mungu,+ mwenye anawaita kwenye Ufalme+ na utukufu wake.+ 13  Kwa kweli, hiyo ndiyo sababu sisi pia tunamushukuru Mungu bila kuacha,+ kwa sababu wakati mulipokea neno la Mungu, lenye mulisikia kutoka kwetu, hamukulikubali kama neno la wanadamu, lakini mulilikubali kama vile liko kwa kweli, kama neno la Mungu, lenye pia linafanya kazi ndani yenu ninyi waamini. 14  Kwa maana, ndugu, ninyi mulikuwa waigaji wa makutaniko ya Mungu yenye kuwa katika Yudea katika umoja na Kristo Yesu, kwa sababu ninyi muliteseka katika mikono ya wanainchi wenzenu,+ kama vile wao pia wanateseka katika mikono ya Wayahudi, 15  wenye hata walimuua Bwana Yesu+ na manabii na kututesa.+ Zaidi ya hayo, hawamupendeze Mungu, lakini wanapinga mambo yenye kuletea wanadamu wote faida, 16  wakati wanajaribu kutuzuia kuwahubiria watu wa mataifa ili waokolewe.+ Kwa njia hiyo, sikuzote wanaendelea kujaza kipimo cha zambi zao. Lakini mwishowe kasirani yake kali imekuja juu yao.+ 17  Hata hivyo, ndugu, wakati tuliachana na ninyi* kwa wakati kidogo tu (kwa mwili, hapana katika mioyo yetu), kwa sababu tulitamani sana kuwaona, tulijikaza sana kukutana na ninyi uso kwa uso.* 18  Kwa sababu hiyo, tulitamani kuja kwenu, ndiyo, mimi Paulo, nilijaribu haiko mara moja tu lakini mara mbili; hata hivyo Shetani alizuia njia yetu. 19  Kwa maana, ni nini tumaini letu ao shangwe ao taji la furaha kubwa mbele ya Bwana wetu Yesu wakati wa kuwapo kwake? Je, kwa kweli haiko ninyi?+ 20  Hakika, ninyi ndio utukufu wetu na furaha yetu.

Maelezo ya Chini

Ao “tukuwe na uhodari.”
Ao pengine, “katika kupambana sana.”
Ao “tunawahimiza.”
Ao “kutuhangaikia.”
Ao “anatunza.”
Ao “upendo mwororo.”
Ao “nafsi yetu.”
Ao “kuhimiza.”
Ao “tuliachwa yatima.”
Tnn., “kuona uso wenu.”