Ya Pili kwa Timoteo 3:1-17

  • Nyakati za hatari katika siku za mwisho (1-7)

  • Fuata mufano wa Paulo kwa ukaribu (8-13)

  • “Endelea kufuata mambo yenye ulijifunza” (14-17)

    • Kila Andiko limeongozwa na roho ya Mungu (16)

3  Lakini ujue jambo hili, kwamba katika siku za mwisho+ kutakuwa nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia.  Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda feza, wenye kujisifu, wenye kujivuna, wenye kumutukana Mungu, wenye hawatii wazazi, wenye hawana shukrani, wenye hawana ushikamanifu,  wenye hawana upendo wa asili, wenye hawataki makubaliano yoyote, wachongezi, wenye hawajizuie, wakali, wenye hawapendi wema,  wasaliti, wenye vichwa vigumu, wenye kujivuna kwa kiburi, wenye kupenda raha kuliko kumupenda Mungu,  wenye kwa inje wanaonekana kuwa na ushikamanifu kwa Mungu lakini wanakana nguvu za ushikamanifu huo;+ na wewe ujiepushe na watu wa namna hiyo.  Katikati ya hao kunainuka watu wenye kujiingiza kwa ujanja katika nyumba na kukamata mateka wanamuke wazaifu wenye kulemewa na mizigo ya zambi, wenye kuongozwa na tamaa mbalimbali,  wenye kujifunza sikuzote lakini hawawezi hata kidogo kupata ujuzi wenye hauna makosa* wa ile kweli.  Basi kwa namna yenye Yane na Yambre walipinga Musa, ni vile hawa pia wanaendelea kupinga kweli. Watu hao wameharibika kabisa katika akili, wakiwa wamekataliwa kuhusiana na imani.  Hata hivyo, hawatafanya maendeleo zaidi, kwa maana upumbavu* wao utaonekana na watu wote, kama vile ilikuwa kwa watu hao wawili.+ 10  Lakini wewe umefuata kwa ukaribu fundisho langu, mwendo wangu wa maisha,+ kusudi langu, imani yangu, subira yangu, upendo wangu, uvumilivu wangu, 11  mateso na shida kama zile zenye nilipata katika Antiokia,+ Ikoniamu,+ na Listra.+ Nilivumilia mateso hayo, na Bwana aliniokoa katika mambo hayo yote.+ 12  Kwa kweli, wale wote wenye wanapenda kuishi maisha ya ushikamanifu kwa Mungu katika umoja na Kristo Yesu watateswa pia.+ 13  Lakini watu waovu na wajanja wataendelea kutoka ubaya mupaka ubaya zaidi, wakipotosha watu na kupotoshwa wao wenyewe.+ 14  Hata hivyo, wewe endelea kufuata mambo yenye ulijifunza na yenye ulisadikishwa kuamini,+ ukijua ulijifunza mambo hayo kutoka kwa nani, 15  na kwamba tangu utoto wako+ umejua maandishi matakatifu,+ yenye yanaweza kukufanya ukuwe mwenye hekima kwa ajili ya wokovu kupitia imani katika Kristo Yesu.+ 16  Kila Andiko limeongozwa na roho ya Mungu+ na liko na faida kwa kufundisha,+ kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo,* kwa kutia ­nizamu ­katika haki,+ 17  ili mutu wa Mungu akuwe na uwezo kamili, akiwa na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.

Maelezo ya Chini

Ao “ujuzi sahihi wa kweli.”
Ao “wazimu.”
Ao “kurekebisha.”