Ya Pili kwa Timoteo 3:1-17
3 Lakini ujue jambo hili, kwamba katika siku za mwisho+ kutakuwa nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia.
2 Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda feza, wenye kujisifu, wenye kujivuna, wenye kumutukana Mungu, wenye hawatii wazazi, wenye hawana shukrani, wenye hawana ushikamanifu,
3 wenye hawana upendo wa asili, wenye hawataki makubaliano yoyote, wachongezi, wenye hawajizuie, wakali, wenye hawapendi wema,
4 wasaliti, wenye vichwa vigumu, wenye kujivuna kwa kiburi, wenye kupenda raha kuliko kumupenda Mungu,
5 wenye kwa inje wanaonekana kuwa na ushikamanifu kwa Mungu lakini wanakana nguvu za ushikamanifu huo;+ na wewe ujiepushe na watu wa namna hiyo.
6 Katikati ya hao kunainuka watu wenye kujiingiza kwa ujanja katika nyumba na kukamata mateka wanamuke wazaifu wenye kulemewa na mizigo ya zambi, wenye kuongozwa na tamaa mbalimbali,
7 wenye kujifunza sikuzote lakini hawawezi hata kidogo kupata ujuzi wenye hauna makosa* wa ile kweli.
8 Basi kwa namna yenye Yane na Yambre walipinga Musa, ni vile hawa pia wanaendelea kupinga kweli. Watu hao wameharibika kabisa katika akili, wakiwa wamekataliwa kuhusiana na imani.
9 Hata hivyo, hawatafanya maendeleo zaidi, kwa maana upumbavu* wao utaonekana na watu wote, kama vile ilikuwa kwa watu hao wawili.+
10 Lakini wewe umefuata kwa ukaribu fundisho langu, mwendo wangu wa maisha,+ kusudi langu, imani yangu, subira yangu, upendo wangu, uvumilivu wangu,
11 mateso na shida kama zile zenye nilipata katika Antiokia,+ Ikoniamu,+ na Listra.+ Nilivumilia mateso hayo, na Bwana aliniokoa katika mambo hayo yote.+
12 Kwa kweli, wale wote wenye wanapenda kuishi maisha ya ushikamanifu kwa Mungu katika umoja na Kristo Yesu watateswa pia.+
13 Lakini watu waovu na wajanja wataendelea kutoka ubaya mupaka ubaya zaidi, wakipotosha watu na kupotoshwa wao wenyewe.+
14 Hata hivyo, wewe endelea kufuata mambo yenye ulijifunza na yenye ulisadikishwa kuamini,+ ukijua ulijifunza mambo hayo kutoka kwa nani,
15 na kwamba tangu utoto wako+ umejua maandishi matakatifu,+ yenye yanaweza kukufanya ukuwe mwenye hekima kwa ajili ya wokovu kupitia imani katika Kristo Yesu.+
16 Kila Andiko limeongozwa na roho ya Mungu+ na liko na faida kwa kufundisha,+ kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo,* kwa kutia nizamu katika haki,+
17 ili mutu wa Mungu akuwe na uwezo kamili, akiwa na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.