Kulingana na Marko 15:1-47

  • Yesu mbele ya Pilato (1-15)

  • Anachekelewa mbele ya watu (16-20)

  • Anatundikwa kwenye muti kule Golgota (21-32)

  • Kifo cha Yesu (33-41)

  • Yesu anazikwa (42-47)

15  Wakati tu wa mapambazuko,* wakubwa wa makuhani, wazee, na waandishi, ndiyo, Sanhedrini yote, wakakusanyika pamoja na kufanya mupango, na wakamufunga Yesu, kisha wakamupeleka na kumutia katika mikono ya Pilato.+  Basi Pilato akamuuliza: “Wewe ndiye Mufalme wa Wayahudi?”+ Akajibu: “Wewe mwenyewe unasema vile.”+  Lakini wakubwa wa makuhani walikuwa wanamushitaki mambo mengi.  Sasa Pilato akaanza tena kumuuliza, na kusema: “Hauna jibu la kutoa?+ Ona namna wanatoa mashitaka mengi juu yako.”+  Lakini Yesu hakutoa jibu lingine, na hivyo Pilato akashangaa.+  Basi, kwenye kila sikukuu, alizoea kuwafungulia mufungwa mumoja mwenye waliomba.+  Wakati huo mutu fulani mwenye kuitwa Baraba alikuwa amefungwa pamoja na watu wengine wenye waliasi serikali, na katika uasi wao walifanya mauaji.  Basi watu wengi wakakuja na kuanza kumuomba Pilato awafanyie kama vile alizoea kuwafanyia.  Akawajibu, na kusema: “Munataka niwafungulie Mufalme wa Wayahudi?”+ 10  Kwa maana Pilato alijua kwamba wakubwa wa makuhani walikuwa wamemutia Yesu katika mikono yake kwa sababu ya wivu.+ 11  Lakini wakubwa wa makuhani wakachochea watu wengi wamuombe Pilato awafungulie Baraba pa nafasi ya Yesu.+ 12  Tena Pilato akawaambia: “Basi, nifanye nini na huyu mwenye munamuita Mufalme wa Wayahudi?”+ 13  Tena wakasema kwa sauti kubwa: “Auawe kwenye muti!”*+ 14  Hata hivyo Pilato akaendelea kuwaambia: “Sababu gani? Amefanya jambo gani la mubaya?” Lakini wakaendelea kusema kwa sauti kubwa zaidi: “Auawe kwenye muti!”*+ 15  Halafu Pilato, kwa kuwa alitaka kufurahisha watu, akawafungulia Baraba; na akaagiza Yesu apigwe mijeledi,+ kisha akamutoa ili auawe kwenye muti.+ 16  Sasa maaskari wakamupeleka katika kiwanja, ni kusema, katika makao ya gavana, na wakakusanya maaskari wote pamoja.+ 17  Wakamuvalisha nguo ya rangi ya zambarau na wakasuka taji la miiba na kuliweka juu yake; 18  Na wakaanza kumuita kwa sauti kubwa: “Jambo, wewe Mufalme wa Wayahudi!”+ 19  Tena, walikuwa wanamupiga kwenye kichwa kwa utete na kumutemea mate, na wakapiga magoti na kuinama mbele yake. 20  Mwishowe, kisha kumuchekelea, wakamuvua ile nguo ya rangi ya zambarau na kumuvalisha nguo zake za inje. Na wakamupeleka inje ili wamupigilie misumari kwenye muti.+ 21  Tena, wakakutana na mupita-njia fulani mwenye kuitwa Simoni wa Kirene, baba ya Aleksanda na Rufo; alikuwa anatoka katika eneo la mashamba. Wakamulazimisha abebe muti wa mateso* wa Yesu.+ 22  Basi wakamupeleka mahali kwenye kunaitwa Golgota, neno lenye wakati linatafsiriwa linamaanisha, “Mahali pa Mufupa wa Kichwa.”+ 23  Na pale wakajaribu kumupatia divai yenye ilitiwa kileo cha manemane,+ lakini hakuikunywa. 24  Wakamupigilia misumari kwenye muti na kugawa nguo zake za inje kwa kuzipigia kura ili kuamua kama kila askari atakamata nini.+ 25  Sasa ilikuwa saa ya tatu (3),* na wakamupigilia misumari kwenye muti. 26  Na maandishi yenye kuonyesha mashitaka kumuhusu yakaandikwa: “Mufalme wa Wayahudi.”+ 27  Zaidi ya hayo, wakaweka wanyanganyi wawili kwenye miti pembeni yake, mumoja upande wake wa kuume na mwingine upande wake wa kushoto.+ 28 * —— 29  Na wapita-njia walikuwa wanamutukana, wakitikisa vichwa vyao+ na kusema: “Aha! Wewe mwenye ulitaka kubomoa hekalu na kulijenga kwa siku tatu (3),+ 30  ujiokoe mwenyewe kwa kushuka kutoka kwenye muti wa mateso.”* 31  Kwa njia ileile pia, wakubwa wa makuhani na waandishi walikuwa wanamuchekelea kati yao, na kusema: “Aliokoa wengine lakini hawezi kujiokoa yeye mwenyewe!+ 32  Sasa Kristo, Mufalme wa Israeli, ashuke sasa kutoka kwenye muti wa mateso,* ili tuone na kuamini.”+ Hata wale wenye walikuwa kwenye miti pembeni yake walikuwa wanamulaumu.+ 33  Wakati ilikuwa saa ya sita (6),* kukakuwa giza juu ya inchi yote mupaka saa ya kenda (9).*+ 34  Na saa ya kenda (9), Yesu akaita kwa sauti kubwa: “Eli, Eli, lama sabaktani?” maneno yenye wakati yanatafsiriwa yanamaanisha: “Mungu wangu, Mungu wangu, sababu gani umeniacha?”+ 35  Na wamoja kati ya wale wenye walikuwa wanasimama karibu, wakati walisikia vile, wakaanza kusema: “Munasikia! Anaita Eliya.” 36  Kisha mutu fulani akakimbia, akalowanisha sifongo* katika divai kali, akaiweka kwenye utete na kumupatia akunywe,+ na kusema: “Mumuache! Tuone kama Eliya atakuja kumushusha.” 37  Lakini Yesu akalia kwa sauti kubwa, na akakufa.*+ 38  Na pazia la patakatifu+ likapasuka vipande mbili kuanzia juu mupaka chini.+ 39  Sasa ule ofisa wa jeshi mwenye alikuwa anasimama pembeni yake akiangalia, wakati aliona amekufa katika hali hizo, akasema: “Hakika mutu huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”+ 40  Kulikuwa pia wanamuke wenye walikuwa wanaangalia kwa mbali, kati yao kulikuwa Maria Magdalene, na pia Maria mama ya Yakobo Mudogo na Yose, na Salome;+ 41  wanamuke hao walikuwa wanamufuata na kumutumikia+ wakati alikuwa Galilaya, na wanamuke wengine wengi wenye walikuwa wamekuja Yerusalemu pamoja naye. 42  Sasa kwa kuwa tayari ilikuwa mangaribi, na kwa kuwa ilikuwa Matayarisho, ni kusema, siku yenye kutangulia Sabato, 43  Yosefu wa Arimatea, mushiriki wa Baraza mwenye kuheshimiwa, mwenye alikuwa pia anangojea Ufalme wa Mungu, akakuja. Akajipatia uhodari, akaingia na kuja mbele ya Pilato na akaomba apewe mwili wa Yesu.+ 44  Lakini Pilato akataka kujua ikiwa alikuwa amekwisha kufa, na akaita ule ofisa wa jeshi, akamuuliza kama Yesu amekwisha kufa. 45  Basi kisha ule ofisa wa jeshi kumuhakikishia, akamuruhusu Yosefu akamate mwili huo. 46  Kisha Yosefu akanunua nguo ya kitani kizuri na kumushusha chini, akamufunga katika ile nguo ya kitani kizuri na kumulalisha katika kaburi*+ lenye lilikuwa limechimbwa katika mwamba; kisha akaviringisha jiwe kwenye muingilio wa lile kaburi.+ 47  Lakini Maria Magdalene na Maria mama ya Yose wakaendelea kuangalia mahali alikuwa amelalishwa.+

Maelezo ya Chini

Mapambazuko ni wakati mwangaza wa asubui unaanza kutokea.
Ao “Umuue kwenye muti.”
Ao “Umuue kwenye muti.”
Ni kusema, karibu saa 3 ya asubui (9:00).
Ni kusema, karibu saa 6 ya muchana-kati (12:00).
Ni kusema, karibu saa 9 kisha muchana-kati (15:00).
Sifongo ni kitu cha teketeke chenye kinaweza kunyonya vitu vya majimaji.
Ao “akakata pumuzi.”
Ao “kaburi la ukumbusho.”