Kulingana na Matayo 13:1-58

  • MIFANO JUU YA UFALME (1-52)

    • Mupandaji (1-9)

    • Sababu gani Yesu alitumia mifano? (10-17)

    • Mufano wa mupandaji unafasiriwa (18-23)

    • Ngano na magugu (24-30)

    • Mbegu ya haradali na chachu (31-33)

    • Kutumia mifano kunatimiza unabii (34, 35)

    • Mufano wa ngano na magugu unafasiriwa (36-43)

    • Hazina yenye ilifichwa na lulu ya muzuri (44-46)

    • Wavu wa kukokota (47-50)

    • Hazina mupya na za zamani (51, 52)

  • Yesu anakataliwa katika eneo la kwao (53-58)

13  Siku hiyo Yesu alitoka katika nyumba na alikuwa amekaa pembeni ya bahari.  Kisha watu wengi sana wakakusanyika karibu naye, basi akaingia katika mashua* na kukaa, na watu wote hao walikuwa wamesimama pembeni ya bahari.+  Kisha akawaambia mambo mengi kwa kutumia mifano,+ kwa kusema: “Muangalie! Mupandaji alienda kupanda mbegu.+  Wakati alikuwa anapanda, mbegu fulani zilianguka pembeni ya barabara, na ndege wakakuja na kuzikula.+  Zingine zilianguka mahali kwenye miamba kwenye hapakukuwa udongo mwingi, na zikaota mara moja kwa sababu udongo haukukuwa mwingi.+  Lakini wakati jua lilitokea, ziliungua na kukauka kwa sababu hazikukuwa na mizizi.  Zingine zilianguka katikati ya miiba, na miiba ikakomaa na kuzifinya.+  Mbegu zingine pia zilianguka kwenye udongo muzuri, na zikaanza kuzaa matunda, hii mara mia moja (100) zaidi, ile mara makumi sita (60), na ile ingine mara makumi tatu (30).+  Ule mwenye kuwa na masikio, asikilize.”+ 10  Basi wanafunzi wakakuja na kumuuliza: “Sababu gani unasema nao kwa kutumia mifano?”+ 11  Akawajibu: “Ninyi mumepewa uwezo wa kuelewa siri takatifu+ za Ufalme wa mbinguni, lakini wao hawakupewa uwezo huo. 12  Kwa maana kila mutu mwenye kuwa na kitu ataongezewa, na atakuwa na mengi zaidi; lakini kila mutu mwenye hana kitu, atanyanganywa hata kile chenye iko* nacho.+ 13  Ndiyo sababu ninasema nao kwa kutumia mifano; kwa sababu wanaangalia, lakini hawaone, na wanasikiliza lakini hawasikie, na hawaelewe maana.+ 14  Na unabii wa Isaya unatimia kwao wenye unasema: ‘Kwa kweli, mutasikia lakini hamutaelewa hata kidogo maana yake, na kwa kweli mutaangalia lakini hamutaona hata kidogo.+ 15  Kwa maana moyo wa watu hawa umekuwa mugumu, na kwa masikio yao wamesikia bila kuitikia, na wamefunga macho yao, ili wasione hata kidogo kwa macho yao na wasisikie kwa masikio yao na wasielewe maana kwa mioyo yao na kugeuka na mimi niwaponyeshe.’+ 16  “Lakini, yenye furaha ni macho yenu kwa sababu yanaona na masikio yenu kwa sababu yanasikia.+ 17  Kwa maana, kwa kweli ninawaambia ninyi, manabii wengi na watu wenye haki walitamani kuona mambo yenye munaona lakini hawakuyaona,+ na kusikia mambo yenye munasikia lakini hawakuyasikia. 18  “Sasa musikilize maana ya mufano wa ule mupandaji.+ 19  Wakati mutu anasikia neno la Ufalme lakini haelewe maana yake, ule muovu+ anakuja na kunyanganya kile kilipandwa katika moyo wake; hiyo ndiyo mbegu yenye ilipandwa pembeni ya barabara.+ 20  Na ile yenye ilipandwa kwenye miamba, huyo ndiye mutu mwenye anasikia neno na mara moja analipokea kwa furaha.+ 21  Hata hivyo, hana mizizi ndani yake lakini anaendelea kwa wakati fulani, na kisha taabu ao mateso kutokea kwa sababu ya lile neno, anakwazika mara moja. 22  Na mbegu yenye ilipandwa katikati ya miiba, huyo ndiye mutu mwenye anasikia neno, lakini mahangaiko ya mupangilio huu wa mambo*+ na nguvu za udanganyifu wa utajiri vinafinya lile neno, na halizae matunda.+ 23  Na mbegu yenye ilipandwa kwenye udongo muzuri, huyo ndiye mutu mwenye anasikia neno na kulielewa, mwenye kwa kweli anazaa matunda na kutoa, huyu mara mia moja (100), ule makumi sita (60), na ule mwingine makumi tatu (30).”+ 24  Akawatolea mufano mwingine, kwa kusema: “Ufalme wa mbinguni unaweza kufananishwa na mutu mwenye alipanda mbegu ya muzuri katika shamba lake. 25  Wakati watu walikuwa wamelala usingizi, adui yake akakuja na kupanda magugu katikati ya ngano kisha akaenda. 26  Wakati mumea uliota na kuzaa matunda, magugu pia yakaonekana. 27  Kwa hiyo watumwa wa bwana wa nyumba wakakuja na kumuambia, ‘Bwana, je, haukupanda mbegu ya muzuri katika shamba lako? Basi, sasa magugu yametoka wapi?’ 28  Akawaambia, ‘Adui, mutu fulani, ndiye alifanya vile.’+ Watumwa wakamuuliza, ‘Unataka basi tuende tuyakusanye?’ 29  Akasema, ‘Hapana, ili, wakati munakusanya magugu, musingoe ngano pia. 30  Muache zote zikomae pamoja mupaka wakati wa mavuno, na katika kipindi cha mavuno nitaambia wavunaji: Mukusanye magugu kwanza na kuyafunga mafungu-mafungu ili kuyachoma katika moto; kisha mukusanye ngano na kuitia katika depo yangu.’”+ 31  Akawatolea mufano mwingine, kwa kusema: “Ufalme wa mbinguni ni kama mbegu ya haradali, yenye mutu alikamata na kupanda katika shamba lake.+ 32  Hiyo kwa kweli, ni ya kidogo sana kuliko mbegu zote, lakini wakati imekomaa, inakuwa ya mukubwa zaidi kati ya mimea ya mboga na inakuwa muti, na ndege wa mbinguni wanakuja na kupata makao katika matawi yake.” 33  Akawaambia mufano mwingine: “Ufalme wa mbinguni ni kama chachu yenye mwanamuke alikamata na kuichanga na vipimo vikubwa tatu (3) vya unga, mupaka tonge lote likavimba.”*+ 34  Yesu aliambia watu wengi mambo yote hayo kwa kutumia mifano. Kwa kweli, hakukuwa anasema nao bila mufano,+ 35  ili kutimiza neno lenye lilisemwa kupitia nabii, mwenye alisema: “Nitafungua kinywa changu kwa mifano; nitatangaza mambo yenye yalifichwa tangu kuwekwa musingi.”*+ 36  Kisha Yesu kuacha wale watu wengi waende, akaingia ndani ya nyumba. Wanafunzi wake wakakuja kwenye alikuwa na kumuambia: “Utuelezee maana ya ule mufano wa magugu katika shamba.” 37  Akawajibu: “Mupandaji wa mbegu ya muzuri ni Mwana wa binadamu; 38  shamba ni ulimwengu.+ Na mbegu ya muzuri, ni wana wa Ufalme, lakini magugu ni wana wa ule muovu,+ 39  na adui mwenye alipanda magugu ni Ibilisi. Mavuno ni umalizio wa mupangilio wa mambo,* na wavunaji ni malaika. 40  Kwa hiyo, kama vile magugu yanakusanywa na kuchomwa katika moto, ni vile itakuwa katika umalizio wa mupangilio wa mambo.*+ 41  Mwana wa binadamu atatuma malaika wake, na watakusanya kutoka katika Ufalme wake vitu vyote vyenye vinafanya watu wakwazike na pia watu wenye matendo ya kuvunja sheria, 42  na watawatupa ndani ya tanuru ya moto.+ Ni mule watalia na kusaga meno yao. 43  Wakati huo wale wenye haki watangaa kama jua+ katika Ufalme wa Baba yao. Ule mwenye kuwa na masikio, asikilize. 44  “Ufalme wa mbinguni ni kama hazina yenye ilifichwa katika shamba, yenye mutu fulani aliona na kuficha tena; na kwa sababu ya furaha yake, akaenda na kuuzisha vitu vyake vyote na kununua shamba hilo.+ 45  “Tena Ufalme wa mbinguni ni kama mufanyabiashara musafiri mwenye kutafuta lulu ya muzuri. 46  Wakati aliona lulu moja yenye samani kubwa, alienda na mara moja akauzisha vitu vyake vyote na kuinunua.+ 47  “Tena Ufalme wa mbinguni ni kama wavu wa kukokotwa wenye ulishushwa* katika bahari na kukusanya samaki wa kila namna. 48  Wakati ulijaa, waliukokotea kwenye inchi kavu, na wakakaa, wakakusanya samaki wazuri+ ndani ya vyombo, lakini wale samaki wenye hawafae+ wakawatupa. 49  Ni vile itakuwa katika umalizio wa mupangilio wa mambo.* Malaika watakuja na kutenganisha waovu kutoka kati ya wenye haki 50  na watatupa waovu ndani ya tanuru ya moto. Ni mule watalia na kusaga meno yao. 51  “Je, mumeelewa maana ya mambo hayo yote?” Wakamujibu: “Ndiyo.” 52  Kisha akawaambia: “Kwa kuwa ni vile, kila mufundishaji wa watu wote mwenye anafundishwa juu ya Ufalme wa mbinguni ni kama mutu fulani, bwana wa nyumba, mwenye anatosha katika depo yake ya hazina vitu vipya na vya zamani.” 53  Wakati Yesu alimaliza mifano hiyo, akatoka pale. 54  Kisha kuingia katika eneo la kwao,+ akaanza kufundisha katika sinagogi lao, mupaka wakashangaa na kusema: “Mutu huyu alipata wapi hekima hii na uwezo wa kufanya matendo haya yenye nguvu?+ 55  Je, huyu haiko mwana wa ule seremala?+ Mama yake haitwe Maria, na ndugu zake Yakobo, Yosefu, Simoni, na Yuda?+ 56  Na dada zake, wote hawako pamoja na sisi? Basi, alipata wapi mambo haya yote?”+ 57  Basi wakaanza kukwazika kwa sababu yake.+ Lakini Yesu akawaambia: “Nabii anaheshimiwa kila mahali isipokuwa katika eneo la kwao na katika nyumba yake mwenyewe.”+ 58  Na hakufanya pale matendo mengi yenye nguvu kwa sababu walikosa imani.

Maelezo ya Chini

Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “eko.”
Ao “mufumo huu wa mambo.” Angalia Maana ya Maneno.
Ao “likachacha.”
Ao pengine, “kuwekwa musingi wa ulimwengu.”
Ao “mufumo wa mambo.” Angalia Maana ya Maneno.
Ao “mufumo wa mambo.” Angalia Maana ya Maneno.
Ao “makila ya kukokotwa yenye ilishushwa.”
Ao “mufumo wa mambo.” Angalia Maana ya Maneno.