Kwa Waroma 14:1-23

  • Musihukumu wengine (1-12)

  • Musikwaze wengine (13-18)

  • Mujikaze kupata amani na umoja (19-23)

14  Mukaribishe mutu mwenye kuwa na uzaifu katika imani yake,+ lakini musitoe hukumu juu ya mawazo yenye kuwa tofauti.*  Mutu mumoja iko* na imani ya kula kila kitu, lakini mutu mwenye kuwa muzaifu anakula mboga za majani tu.  Ule mwenye anakula asimuzarau ule mwenye hakule, na ule mwenye hakule asimuhukumu ule mwenye anakula,+ kwa maana Mungu amemukaribisha.  Wewe ni nani ili umuhukumu mutumishi wa mwingine?+ Kwa bwana wake anasimama ao anaanguka.+ Kwa kweli, atasimamishwa, kwa maana Yehova* anaweza kumusimamisha.  Mutu mumoja anahukumu siku moja kuwa ya maana kuliko ingine;+ mwingine anahukumu siku moja kuwa sawa na siku zingine zote;+ kila mutu asadikishwe kikamili katika akili yake mwenyewe.  Ule mwenye anashika siku anaishika kwa ajili ya Yehova.* Pia, ule mwenye anakula, anakula kwa ajili ya Yehova,* kwa maana yeye anamushukuru Mungu;+ na ule mwenye hakule, hakule kwa ajili ya Yehova,* na bado yeye anamushukuru Mungu.+  Kwa kweli, hakuna hata mumoja wetu mwenye anaishi kwa ajili yake mwenyewe tu,+ na hakuna mutu yeyote mwenye anakufa kwa ajili yake mwenyewe tu.  Kwa maana kama tunaishi, tunaishi kwa ajili ya Yehova,*+ na kama tunakufa, tunakufa kwa ajili ya Yehova.* Basi kama tunaishi na kama tunakufa, sisi ni wa Yehova.*+  Kwa maana kwa kusudi hili Kristo alikufa na akarudia tena ­kwenye uzima, ili akuwe Bwana juu ya wafu na pia juu ya wazima.+ 10  Lakini sababu gani unamuhukumu ndugu yako?+ Ao sababu gani pia unamuzarau ndugu yako? Kwa maana sisi wote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Mungu.+ 11  Kwa maana imeandikwa: “‘Kama vile hakika ninaishi,’+ Yehova* anasema, ‘kila goti litapigwa mbele yangu, na kila ulimi utakubali Mungu waziwazi.’”+ 12  Kwa hiyo basi, kila mumoja wetu atatoa hesabu kwa Mungu kwa ajili yake mwenyewe.+ 13  Kwa hiyo, tusikuwe tunahukumiana tena,+ lakini, tofauti na hilo, mufanye nguvu yenu yote ili musiweke kikwazo ao kizuizi mbele ya ndugu.+ 14  Ninajua na ninasadiki katika Bwana Yesu kwamba hakuna kitu chenye kiko kichafu ndani yacho chenyewe;+ isipokuwa wakati mutu anaona kitu fulani kuwa kichafu, kwake yeye kinakuwa kichafu. 15  Kwa maana kama ndugu yako anakasirika kwa sababu ya chakula, wewe hautembee tena kulingana na upendo.+ Kupitia chakula chako usimuharibu ule mwenye Kristo alikufa kwa ajili yake.+ 16  Kwa hiyo, musiache mambo ya muzuri yenye munafanya yasemwe kuwa ni mambo ya mubaya. 17  Kwa maana Ufalme wa Mungu haumaanishe kula na kunywa,+ lakini unamaanisha haki, amani, furaha pamoja na roho takatifu. 18  Kwa maana mutu yeyote mwenye anamutumikia Kristo kwa njia hiyo ni mwenye kupendeza mbele ya Mungu na anakubaliwa na wanadamu. 19  Kwa hiyo basi, tufuatilie mambo yenye yanafanya kukuwe amani+ na mambo ya kujengana mumoja na mwingine.+ 20  Muache kubomoa kazi ya Mungu kwa ajili ya chakula tu.+ Ni kweli, vitu vyote viko safi, lakini ni mubaya* kwa mutu kula kama kufanya vile kutakwaza.+ 21  Ni muzuri zaidi kuacha kula nyama ao kunywa divai ao kufanya jambo lolote lenye linamukwaza ndugu yako.+ 22  Imani yenye uko nayo, ukuwe nayo kwa ajili yako wewe mwenyewe mbele ya Mungu. Mwenye furaha ni mutu mwenye hajihukumu yeye mwenyewe ­kupitia mambo yenye ­anakubali. 23  Lakini ikiwa iko* na mashaka, kama anakula tayari amehukumiwa kuwa na kosa, kwa sababu hakule kwa kutegemea imani. Kwa kweli, kila kitu chenye hakitegemee imani ni zambi.

Maelezo ya Chini

Ao pengine, “maulizo ya ndani.”
Ao “eko.”
Ao “kosa.”
Ao “eko.”