Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAWAZO YA BIBLIA

Mbingu

Mbingu

Neno mbingu linatokeza mawazo mengi ya kuwazia na pia ubishi mukali. Lakini, mambo yenye Biblia inafundisha juu ya mbingu ni tofauti kabisa na mambo yenye watu wengi wamefundishwa.

Mbingu ni nini?

MAMBO WATU FULANI WANASEMA

Kuko mafundisho mengi juu ya mbingu na kusudi lake. Kwa mufano:

  • Wengi wenye kujiita Wakristo wanaweza kuitika mambo kitabu kimoja cha Kikatoliki kinasema. Kitabu hicho kinaita mbingu “makao ya mwisho ya wabarikiwa wenye wanakufa katika Bwana.”(New Catholic Encyclopedia)

  • Rabbi Bentzion Kravitz anasema hivi: “Dini ya Kiyahudi inakazia sana maisha ya sasa kuliko maisha ya kisha mutu kufa.” Lakini anaonyesha kama, “mbinguni nafsi inakuwa na furaha nyingi sana, ni kusema, inajisikia na kujiona kuwa karibu sana na Mungu kuliko wakati wa mbele.” Hata hivyo, Kravitz anasema kuwa, “hata kama dini ya Kiyahudi inaamini mbingu, Torati (vitabu tano vya kwanza vya Biblia) haizungumuzie sana mbingu.”

  • Wahindu na Wabuda wanaamini kama mbingu iko na makao mengi ya kiroho. Ni mahali pa muda, kisha hapo mutu anazaliwa tena kwenye dunia ao anaenda katika Nirvana, ni kusema, hali ya juu sana kuliko mbingu.”

  • Watu fulani wanakataa mawazo yote ya dini juu ya mbingu na wanasema kama wazo hilo la mbingu ni la kitoto na halina maana.

Neno mbingu linatokeza mawazo mengi ya kuwazia

MAMBO BIBLIA INAFUNDISHA

Katika Biblia, neno “mbingu” linamaanisha mambo mengi. Kwa mufano:

  • Andiko la Mwanzo 1:20 linazungumuzia uumbaji wa ndege wenye ‘kuruka juu ya dunia kwenye uso wa anga la mbingu.’ Katika andiko hilo, neno “mbingu” linamaanisha angahewa letu, ni kusema, anga lenye tunaona kwa macho.

  • Andiko la Isaya 13:10 linataja “nyota za mbinguni na makundi-nyota yake,” ni kusema, anga la juu sana.

  • Biblia inazungumuzia “makao [ya Mungu] mbinguni” na inasema juu ya malaika wenye kuwa “mbinguni.” (1 Wafalme 8:30; Mathayo 18:10) Ona kama neno “mbinguni” haliko tu neno la mufano lakini linamaanisha makao ya kweli kabisa. *

“Tazama kutoka mbinguni, uone kutoka katika makao yako yaliyoinuliwa ya utakatifu na uzuri.”Isaya 63:15.

Watu wote wazuri wanaenda mbinguni wakati wanakufa?

Biblia haifundishe kama dunia ni makao ya muda kwenye watu wanangojea kifo na kisha wanaenda kuishi mbinguni. Biblia inaonyesha waziwazi kama katika kusudi la Mungu la mwanzoni, hakupenda watu wakufe. Ona mambo yenye kufuata:

  • Mungu aliambia mwanaume na mwanamuke wa kwanza hivi: ‘Muzae, mukuwe wengi, mujaze dunia.’ (Mwanzo 1:28) Dunia ilipaswa kuwa makao ya milele ya mwanadamu, kwenye angeweza kuishi milele. Mwanaume na mwanamuke wa kwanza wangekufa kama tu wangekosa kumutii Mungu. Jambo la huzuni ni kwamba, waliamua kukosa kumutii Mungu.—Mwanzo 2:17; 3:6.

  • Kukosa kutii kwa mwanaume wa kwanza kulimuletea kifo yeye na bibi yake na hata watoto wao. (Waroma 5:12) Hilo lilifanya wanadamu wakose tumaini?

  • Biblia inasema kama, ‘kulingana na ahadi yake [Mungu] tunangojea mbingu mupya na dunia mupya, na humo uadilifu [haki] utakaa.’ * (2 Petro 3:13) Kupitia Ufalme wake, Mungu atarudishia dunia hii hali yenye alikusudia ikuwe nayo, “na kifo hakitakuwapo tena.” (Ufunuo 21:3, 4) Andiko hilo linazungumuzia maisha ya mbinguni ao maisha kwenye dunia? Ili kitu fulani ‘kisikuwe tena’ mahali fulani, kinapaswa kuwa kilikuwa hapo kwanza. Lakini, kifo hakijakuwaka mbinguni. Kwa hiyo, andiko hilo linazungumuzia mambo yenye yatafanyika kwenye dunia, mahali tulikusudiwa kuishi na kwenye tunatamani kuwa pamoja na wapendwa wetu. Tena, Biblia inaonyesha kama watu waliokufa watafufuliwa na wataishi tena pamoja na wapendwa wao.—Yohana 5:28, 29.

Watu wengi wamefurahi sana kwa kujifunza mambo Biblia inafundisha kabisa juu ya mbingu. Kwa mufano, George, mwenye alikuwa Mukatoliki, anasema hivi: “Nilivumbua kama fundisho la Biblia juu ya kuishi milele kwenye dunia ni lenye kutuliza. Fundisho hilo linaeleweka zaidi kuliko fundisho la kuenda mbinguni.” *

“Mbingu ni mbingu za Yehova, bali [lakini] dunia amewapa wana wa binadamu.”Zaburi 115:16.

^ fu. 13 Kwa kweli, Mungu ana mwili wa kiroho, hana mwili kama wetu. (Yohana 4:24) Kwa hiyo, makao yake yanapaswa kuwa makao ya kiroho yenye kuwa tofauti na ulimwengu wetu wenye kuonekana.

^ fu. 19 Neno ‘dunia mupya’ haiko sayari (planète) mupya; lakini ni neno la mufano lenye kumaanisha watu wenye wanakubaliwa na Mungu ambao wataishi kwenye dunia.—Zaburi 66:4.

^ fu. 20 Biblia inafundisha kama, ni watu kidogo tu ndio walichaguliwa ili kutawala na Yesu mbinguni katika Ufalme wa Mungu. Hesabu yao ni watu 144000.—1 Petro 1:3, 4; Ufunuo 14:1.