Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Utambulisho wako wenye nguvu, utakusaidia uokoke wakati wa upepo mukali

KWA AJILI YA VIJANA

9: Utambulisho

9: Utambulisho

MAANA YAKE NINI?

Utambulisho wako haiko tu jina na namna unaonekana, lakini unatia ndani mambo mengi zaidi. Unatia ndani kanuni za mwenendo zenye unafuata, mambo yenye unaamini, na tabia zako. Kwa kweli, utambulisho wako ni jambo lolote lenye linafanya ukuwe kile uko; ndani na inje.

SABABU GANI NI JAMBO LA MAANA

Ikiwa unatambua kabisa kile uko, utatetea mambo yenye unaamini kuliko kuacha vijana wenzako wakuongoze.

“Watu wengi wako kama sanamu za kuonyesha nguo zenye kupatikana nafasi ya kuuzishia. Hazichague manguo yenye zinavaa; ni wengine ndio wanazichagulia.”​—Adrian.

“Nimejifunza namna ya kutetea mambo yenye kuwa sawa hata kama ni nguvu kufanya hivyo. Ninaweza kujua marafiki wangu ni nani kabisa kwa kuona namna wanatenda na namna ninatenda wakati niko pembeni yao.”​—Courtney.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Muache kufanyizwa kulingana na mufumo huu wa mambo, bali [ao, lakini] mugeuzwe kwa kufanya upya akili yenu.’​—Waroma 12:2.

MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA

Ujikaze kuelewa kile uko kwa sasa na kile unapenda kuwa kwa kuchunguza uwezo wako mbalimbali, uzaifu wako, na mambo yenye unaamini. Njia ya muzuri ili kuanza kufanya hivyo ni kujibia maulizo yenye kufuata.

Uwezo: Ninajua ufundi gani? Niko na sifa gani za muzuri? (Kwa mufano: Ninaheshimia wakati? ninajizuia? ninatumika kwa bidii? niko mukarimu?) Ni mambo gani ya muzuri ninafanyaka?

SHAURI: Je, uko na magumu ya kutambua mambo ya muzuri yenye ulifanya ao kusema? Uliza muzazi wako ao rafiki mwenye kutumainika akuambie uwezo mbalimbali wenye uko nao na sababu gani.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Kila mumoja na asibitishe [ao, achunguze] kazi yake mwenyewe ni nini, kisha atakuwa na sababu ya kufurahi kwa habari yake mwenyewe peke yake, na si kwa kujilinganisha na mutu yule mwingine.’​—Wagalatia 6:4.

Uzaifu: Ni sifa gani niko na lazima ya kufanyia maendeleo zaidi? Ni wakati gani ninajaribiwa sana kufanya mambo ya mubaya? Ni katika mambo gani niko na lazima ya kujizuia zaidi?

KANUNI YA BIBLIA: “Kama tukisema: ‘Sisi hatuna zambi yoyote,’ tunajipotosha wenyewe.”​—1 Yohana 1:8.

Mambo yenye unaamini: Ni kanuni gani za mwenendo ninafuata, na sababu gani? Ninamuamini Mungu? Ni nini imenihakikishia kama Mungu iko kabisa? Ni matendo gani ninaona kuwa haiko ya haki, na sababu gani? Ninaamini mambo gani juu ya wakati wenye kuja?

KANUNI YA BIBLIA: “Uwezo wa kufikiri utakutunza, utambuzi utakulinda.”​—Methali 2:11.