Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kuna Tofauti Gani Kati ya Mwili Kukataa Chakula na Tumbo Kukataa Chakula?

Kuna Tofauti Gani Kati ya Mwili Kukataa Chakula na Tumbo Kukataa Chakula?

Emily anasema hivi: “Kisha kula chakula, nilianza kujisikia mubaya. Kinywa changu kilianza kuwasha, na ulimi wangu ulianza kuvimba. Nilianza kusikia kizunguzungu na sikuweza tena kupumua muzuri. Upele ulianza kuniota kwenye mikono na shingo. Nilipima kujizuia ili nisikuwe na woga, lakini nilijua kwamba nilipaswa kuenda kwenye hospitali bila kukawia!”

KWA watu wengi, kula chakula ni jambo lenye kufurahisha. Lakini, watu fulani wanalazimika kuona chakula fulani kuwa “adui.” Kama vile Emily mwenye tumetaja, watu hao wako na magumu ya mwili kukataa chakula. Hali hiyo ya mubaya sana yenye ilimufikia Emily inaitwa anaphylaxie, ni kusema, mwili unaonyesha alama za mubaya kisha tu kutumia chakula fulani. Jambo la kufurahisha ni hili: hali za mingi haziko za mubaya sana.

Katika miaka ya hivi karibuni, ripoti nyingi zimeonyesha kwamba hesabu ya watu wenye kuwa na magumu ya mwili kukataa chakula na tumbo kukataa chakula inaongezeka. Kulingana na uchunguzi mbalimbali, watu fulani waliwaza kama walikuwa na magumu ya mwili kukataa chakula fulani. Lakini kisha kuona wanganga, ni watu kidogo tu ndio walikuwa na magumu hayo.

Inamaanisha Nini Mwili Kukataa Chakula?

Ripoti moja ya wanasayansi wenye waliongozwa na Munganga Jennifer Schneider Chafen inasema hivi: “Hakuna mafasirio yenye watu wote wanaitika juu ya mwili kukataa chakula.” (The Journal of the American Medical Association) Lakini, watu wengi wenye elimu wanaamini kama jambo la kwanza lenye linafanya mwili ukatae chakula fulani ni uwezo wa mwili wa kujikinga wenyewe.

Kwa kawaida, mwili unakataa chakula kwa sababu ya protini fulani yenye kuwa ndani ya chakula hicho. Uwezo wa mwili wa kujikinga wenyewe unadanganyika kwa kuona protini hiyo kuwa hatari kwa mwili. Wakati protini fulani inaangia katika mwili, uwezo wa mwili wa kujikinga wenyewe unaweza kutengeneza aina fulani ya kinga ya mwili yenye kuitwa IgE (Immunoglobuline E) ili kufanya protini hiyo isikuwe hatari. Wakati unakula tena chakula hicho chenye mwili wako unakataa, kinga za mwili zenye tayari zimetengenezwa zinaweza kutokeza kemikali nyingi na histamine pia.

Katika hali za kawaida, histamine inafanya kazi ya maana katika uwezo wa mwili wa kujikinga wenyewe. Lakini juu ya sababu zenye hazijulikane muzuri, kinga za mwili zenye kuitwa IgE pamoja na histamine zinaletea magumu watu wenye mwili wao unakataa protini fulani yenye kuwa ndani ya chakula.

Ndiyo maana mutu anaweza kula chakula mara ya kwanza bila kupata kabisa magumu, lakini wakati anakula chakula hicho tena kinamuletea magumu.

Inamaanisha Nini Tumbo Kukataa Chakula?

Tumbo kukataa chakula na mwili kukataa chakula vinafanana kwa njia fulani, ni kusema, chakula fulani kinaleta magumu. Lakini, tofauti na mwili kukataa chakula (yenye inatokana na uwezo wa mwili wa kujinga wenyewe), tumbo kukataa chakula inatokana na uwezo wa mwili wa kusaga chakula; kwa hiyo, haiko kinga za mwili zinafanya tumbo ikatae chakula. Kwa kawaida, mutu anaweza kushindwa kusaga chakula, kwa sababu mwili wake uko na kimengenya (enzyme) ndogo ao kwa sababu katika chakula munapatikana kemikali fulani zenye inakuwa vigumu kusaga. Kwa mufano, tumbo inakataa maziwa wakati uwezo wa mwili wa kusaga chakula hautokeze vimengenya vya kutosha ili kusaidia mwili utumie sukari yenye kuwa katika maziwa hayo.

Kwa sababu jambo hilo halitokane na kinga za mwili, tumbo kukataa chakula inaweza kuonyesha matokeo fulani kisha kula chakula kwa mara ya kwanza. Wakati fulani inaweza kutokana na uwingi wa chakula. Pengine wakati mutu anakula chakula kidogo jambo hilo haliwezi kuleta magumu, lakini wakati anakula chakula mingi hilo linaweza kuleta magumu. Jambo hilo ni tofauti na mwili kukataa chakula, kwa sababu hata chakula kidogo sana kinaweza kutia mutu katika hali yenye kuogopesha.

Alama Ni Gani?

Kama mwili wako unakataa chakula fulani, unaweza kuonyesha alama kama vile: mwili kuwasha; kuvimba koo, macho, ao ulimi; kutaka kutapika; kutapika; ao kuhara. Na katika hali fulani ya mubaya zaidi mwendo wa damu unaweza kupunguka, unaweza kuwa na kizunguzungu, kupoteza ufahamu, na hata moyo unaweza kuacha kupiga. Anaphylaxie inaweza kuongezeka mbiombio na kuwa hatari sana.

Kwa kawaida, mwili unaweza kukataa chakula chochote. Lakini, mara nyingi chakula chenye mwili unakataa ni maziwa, mayai, samaki, viumbe vidogo-vidogo vyenye kuishi ndani ya maji (crustacés), kalanga, soya, kokwa (noix), na ngano. Mutu anaweza kujikuta katika hali hiyo hata akuwe na miaka ngapi. Uchunguzi mbalimbali unaonyesha kwamba mara nyingi mutu anariti hali hiyo, na mutoto anaweza kuionyesha zaidi sana kama muzazi wake mumoja ao wote wawili wako nayo. Mara nyingi, wakati watoto wanakomaa mwili wao unaacha kukataa chakula hicho.

Alama zenye mutu anaonyesha wakati tumbo inakataa chakula haziko zenye kuogopesha sana kama zile zenye mutu anaonyesha wakati mwili unakataa chakula. Wakati tumbo inakataa chakula fulani, hilo linaweza kutokeza maumivu ya tumbo, tumbo kuvimba, kutosha gaze, crampes, maumivu ya kichwa, upele wenye kuwasha, muchoko, ao kusikia mwili mubaya. Tumbo kukataa chakula inaweza kutokana na aina mbalimbali ya vyakula, zaidi sana ngano, gluten, pombe, chachu, na vyakula vyenye kutokana na maziwa.

Uchunguzi na Matunzo

Kama unawaza mwili wako unakataa chakula ao tumbo yako inakataa chakula, pengine unaweza kuamua kumuona munganga. Kuamua kukataa chakula fulani kwa sababu umetambua wewe mwenyewe kwamba kinakuletea magumu kunaweza kuwa na matokeo mabaya juu ya afya yako, kwa kuwa unaweza kukataa bure chakula chenye kingejenga mwili wako.

Hakuna matunzo yenye kujulikana sana, isipokuwa tu kuamua kukataa chakula fulani chenye mwili unakataa. * Lakini, kama hali yako haiko nguvu kabisa, unaweza tu kuamua usikule chakula fulani kwa ukawaida ao kula tu chakula kidogo. Katika njia fulani, wale wenye kuteseka kwa sababu ya chakula fulani wanaamua kukataa chakula hicho, ao kukikataa kwa muda fulani, kulingana na hali ya kila mutu.

Kwa hiyo, kama mwili wako unakataa chakula ao tumbo yako inakataa chakula utatiwa moyo kujua kwamba wale wenye kuwa na magumu hayo wamejifunza namna ya kuishi nayo, na wanaendelea kufurahia chakula mbalimbali na chenye kujenga mwili.

^ fu. 19 Wale wenye kupata magumu makali kwa sababu mwili wao unakataa chakula wanashauriwa kutembea na dawa fulani yenye kuwa na adrenalini (epinephrine), yenye mutu anaweza kujitoboa wakati anajikuta katika hali fulani yenye inaomba kutunzwa haraka. Wanganga fulani wa afya wanaona ni muzuri watoto wenye mwili wao unakataa chakula fulani wakuwe na alama ya kutambulisha hali yao mbele ya walimu ao watu wenye kuwachunga.