Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUSAADA KWA FAMILIA | NDOA

Namna ya Kutumia Feza Vizuri

Namna ya Kutumia Feza Vizuri

TATIZO

Wakati unatazama vikaratasi vyako vya benki na garama ambazo inafaa ulipe utaona ni kama vile unabeba feza katika mufuko wenye kutoboka. Hamujakawia katika ndoa, na hamujajua namna ya kutumia feza vizuri. Kosa ni la bibi ao la bwana? Hakuna mwenye anajua! Mufikiri pamoja, na mutafute kujua mambo ambayo yamewaingiza ninyi wawili katika magumu hayo. *

SABABU GANI TATIZO HILO LINATOKEA

Mawazo Tofauti Juu ya Kutumia Feza. Ikiwa ulikuwa unaishi kwenu mbele ya kuoa ao kuolewa, linaweza kuwa jambo geni kwako kulipa garama mbalimbali pamoja na mutu mwengine. Pengine wewe na mwenzako wa ndoa muna mawazo yanayotofautiana juu ya feza. Kwa mufano, pengine mumoja ana muelekeo wa kutumia sana feza, lakini mwengine anapenda kuweka feza kwa ajili ya wakati unaokuja. Inaomba wakati ili bibi na bwana wapatanishe mawazo yao na kukubaliana juu ya namna ya kutumia feza.

Kama majani ambayo inaomba uongoe katika shamba, deni ambayo haujalipa itaendelea tu kukungojea

Kuchelewesha Mambo. Mufanyabiashara mumoja anayeitwa Jim, anakubali kwamba muda mufupi kisha kuoa, kutokujua kupanga mambo vizuri kulimufanya atumie feza nyingi. Anasema hivi: “Kwa sababu nilichelewa kulipa garama mbalimbali, mwishowe mimi na bibi yangu tulilazimika kulipa feza nyingi. Kwa hiyo, feza zilituishia!”

Mutego wa Kutumia “Feza Zenye Hauone.” Ni rahisi kutumia feza nyingi wakati hauna feza katika mikono yako. Inaweza kuwa hivyo ikiwa mara nyingi unanunua vitu kwa kutumia kadi ya mukopo, unanunua vitu kupitia Internete, na mufumo wa benki wa kielektroniki. Uwezekano wa kujikopesha feza kwa vyepesi unaweza kufanya iwe vyepesi kwa watu wanaotoka kuoana hivi karibuni kutumia feza nyingi sana.

Hata sababu iwe nini, feza zinaweza kuleta matatizo makubwa katika ndoa yako. Kitabu kimoja kinasema kwamba “bibi na bwana wengi wanasema kuwa feza ndio tatizo lao kubwa, hata wawe na feza nyingi namna gani, kila mara feza zinawafanya wabishane.” MAMBO AMBAYO UNAWEZA KUFANYA

Muwe tayari kupanga mambo pamoja. Kuliko kutupia mwengine kosa, mupange pamoja namna munaweza kutumia vizuri feza zenu. Mwanzoni mwa mazungumuzo yenu, mukubaliane kwamba hamutaruhusu mambo ya feza iwafanye mubishane.—Kanuni ya Biblia: Waefeso 4:32.

Mupange namna mutatumia feza zenu. Muandike garama zote ambazo mutafanya kwa mwezi mumoja. Hilo litawasaidia kutambua ni wapi feza zenu zinaenda na garama zisizokuwa za lazima. Jim, ambaye tulitaja hapo juu, anasema kwamba “unapaswa kuzuia damu isiendelee kuvuya. Huo ni musemwa unaotumiwa katika mambo ya kiganga na ya biashara.”

Andika garama za maana, kama vile chakula, nguo, feza za kulipia nyumba, motokari, na mambo mengine. Andika bei ya kila kitu, fikiria feza ambazo unaweza kupata kisha siku fulani ao kisha mwezi mumoja.—Kanuni ya Biblia: Luka 14:28.

‘Mukopaji ni mutumishi wa mutu anayemukopesha.’—Methali 22:7

Kila mwezi, panga kiasi cha feza ambacho utatumia kwa ajili ya kila kitu, kwa mufano, chakula, nyumba, na vitu vingine. Wengine wanafanya hivyo kwa kutia feza katika bahasha mbalimbali, kila bahasha kwa ajili ya garama fulani. * Ikiwa feza zinapunguka katika bahasha fulani, wanaweza kuacha kutumia feza zinazobakia ndani ao wanaweza kuhamishia ndani feza zilizo katika bahasha ingine.

Badilisha mawazo yako juu ya vitu. Furaha haitokane na kuwa na vitu vya kisasa. Kumbuka kwamba, Yesu alisema hivi: ‘Hata wakati mutu ana vitu vingi uzima wake hautokane na vitu alivyo navyo.’ (Luka 12:15) Mara nyingi, namna yako ya kutumia feza inaonyesha kama unaamini maneno hayo ao hapana.—Kanuni ya Biblia: 1Timotheo 6:8.

Fanya Mabadiliko. Aaron, ambaye ameoa tangu miaka miwili sasa, anasema hivi: “Mambo kama vile programu za televizyo za kulipia kila mwezi na kuenda kula kwenye restora inaweza kuonekana kuwa yenye kufaa mwanzoni, lakini baadaye inaweza kuingiza mutu katika matatizo ya feza. Ni vizuri tujifunze kuachana na vitu fulani ili kuishi kulingana na uwezo wetu.”

^ fu. 4 Ijapokuwa habari hii inahusu zaidi sana watu ambao wameoana hivi karibuni, kanuni ambazo inazungumuzia zinahusu pia watu waliooana zamani.

^ fu. 13 Ikiwa unalipa feza kwa njia ya kielektroniki ao kupitia kadi ya mukopo, andika garama ambazo ulifanya na uziweke katika kila bahasha.