Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI FULANI ZA ULIMWENGU

Habari Fulani Juu ya Familia

Habari Fulani Juu ya Familia

Familia zinapambana na magumu mengi, lakini hekima ya Biblia yenye kutumika sikuzote inaweza kusaidia familia zishinde magumu hayo na ziendelee kuwa zenye nguvu.

AFRIKA

Kulingana na Shirika la Afya Ulimwenguni (OMS), mama wanapaswa kunyonyesha watoto wao mbele ya saa moja kisha kuzaliwa na kuwanyonyesha kwa muda wa miezi sita bila kuwapatia chakula kingine. Mutu mumoja wa shirika la UNICEF mwenye kutoa mashauri juu ya chakula katika Afrika ya Mashariki na ya Kusini alisema kuwa, hata kama shirika la OMS limetoa shauri hilo, matangazo ya uongo yanaendelea kukazia kwamba, “maziwa yenye kutengenezwa ili kulisha watoto ni ya muzuri kama maziwa ya mama.”

MAMBO BIBLIA INASEMA: ‘Mutu asiye na uzoefu anaamini kila neno, lakini mutu mwerevu anazifikiria hatua zake.’—Methali 14:15.

KANADA

Wachunguzi katika muji wa Montreal wameonyesha kama watoto 30 juu ya 100 wenye wazazi wao ni wakali sana na wanawawekea sheria nyingi ngumu, lakini wanawaonyesha upendo kidogo, wanaweza kunenepa sana kupita watoto wenye wazazi wao wako na usawaziko katika kuonyesha upendo na kufundisha adabu.

ULIJUA? Namna ya kulea watoto yenye kuwaletea faida zaidi ilionyeshwa katika Biblia miaka mingi iliyopita.—Wakolosai 3:21.

UHOLANZI

Uchunguzi wenye ulifanywa juu ya familia za Waholanzi zenye wazazi wote wako na kazi ulionyesha kama wazazi wenye hawachange kazi na madaraka yao ya familia, walikuwa na urafiki wa muzuri pamoja na watoto wao, kuliko wazazi wenye waliacha kazi iwazuie kutimiza madaraka yao ya familia. Kwa mufano, kama muzazi anachanga mambo ya kazi na ya familia kwa kuita-ita kwenye telefone juu ya mambo ya kazi wakati anakuwa nyumbani kisha saa za kazi, hilo linaweza kumuzuia kuhangaikia watoto wake.

JAMBO LA KUFIKIRIA: “Kuna wakati uliowekwa [muzuri zaidi] wa kila kitu.”—Mhubiri 3:1.