Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Walijitoa kwa Kujipendea​​—Katika Myanmar

Walijitoa kwa Kujipendea​​—Katika Myanmar

“MAVUNO ni mengi, lakini wafanyakazi wako kidogo. Kwa hiyo mumuombe Bwana wa mavuno atume wafanyakazi katika mavuno yake.” (Lu. 10:2) Maneno hayo yenye Yesu alisema kumepita miaka 2 000 hivi yanaonyesha muzuri hali yenye kuwa katika Myanmar leo. Sababu gani? Katika Myanmar, kuko tu wahubiri 4 200 hivi wenye kuhubiria watu milioni 55 habari njema.

Lakini, Yehova, “Bwana wa mavuno,” amegusa mioyo ya mamia ya ndugu na dada kutoka katika inchi mbalimbali, na wamekuja katika inchi hii ya Kusini-Mashariki mwa Asia ili kusaidia katika mavuno ya kiroho. Ni nini iliwachochea watoke katika inchi zao? Ni nini iliwasaidia kuhamia katika inchi ya Myanmar? Na wanapata baraka gani? Tuone basi.

“MUKUJE, TUKO NA LAZIMA YA MAPAINIA ZAIDI!”

Miaka fulani yenye ilipita, Kazuhiro, painia mumoja katika Japani, alianguka kwa sababu ya ugonjwa wa kifafa, akapoteza ufahamu, na kupelekwa kwenye hospitali. Munganga alimuambia afanye miaka mbili bila kutembeza gari. Kazuhiro alihuzunika sana. Alijiuliza hivi: ‘Namna gani nitaendelea kufanya kazi yenye ninapenda, ni kusema, upainia?’ Alisali kwa bidii ili kumuomba Yehova amufungulie njia ili aendelee kufanya kazi ya upainia.

Kazuhiro na Mar

Kazuhiro anasema hivi: “Kisha mwezi moja, rafiki yangu mwenye alikuwa anatumikia katika Myanmar alisikia habari juu ya magumu yangu. Aliniita na kusema hivi: ‘Katika Myanmar watu wengi wanatumia bisi ili kusafiri. Kama unakuja huku, unaweza kuendelea na kazi yako ya kuhubiri bila kuwa na lazima ya gari!’ Nilimuuliza munganga wangu ikiwa hali yangu ingeniruhusu niende Myanmar. Nilishangaa sana wakati munganga huyo alisema hivi: ‘Munganga mumoja wa ubongo kutoka Mynmar anatembelea Japani sasa. Nitakutambulisha kwake. Kama unaanguka tena kwa sababu ya kifafa anaweza kukutunza.’ Niliona maneno ya munganga huyo kuwa jibu kutoka kwa Yehova.”

Bila kukawia, Kazuhiro alitumia biro ya tawi ya Myanmar ujumbe kupitia Enternete ili kuwajulisha kama yeye na bibi yake walipenda kufanya kazi ya upainia katika inchi hiyo. Siku tano tu kisha hapo, biro ya tawi ilijibu hivi: “Mukuje, tuko na lazima ya mapainia zaidi!” Kazuhiro na bibi yake, Mari, waliuzisha magari yao, walipata visa zao na wakauza tiketi za ndege. Leo, wanatumika kwa furaha katika kikundi cha luga ya ishara katika Mandalay. Kazuhiro anasema hivi: “Tunaona kama jambo hilo limetia nguvu imani yetu katika ahadi hii ya Mungu yenye kupatikana katika Zaburi 37:5: ‘Tia njia yako katika mukono wa Yehova; umutegemee yeye, naye atatenda kwa ajili yako.’”

YEHOVA ANAFUNGUA NJIA

Katika mwaka wa 2014, Mashahidi wa Yehova katika Myanmar walipata pendeleo la kufanya mukusanyiko wa pekee. Ndugu na dada wengi kutoka katika inchi mbalimbali walikuja kwenye mukusanyiko huo. Mumoja kati yao ni Monique, dada mumoja mwenye alitoka katika inchi ya Amerika, mwenye kuwa na miaka 34, anasema hivi: “Kisha kutoka kwenye mukusanyiko, nilisali kwa Yehova juu ya hatua ingine yenye nilipaswa kufanya katika maisha yangu. Pia, nilizungumuza na wazazi wangu kuhusu miradi yangu ya kiroho. Tuliona kama nilipaswa kurudia Myanmar, lakini iliomba wakati na sala nyingi ili nifikie uamuzi wangu wa mwisho.” Monique anaeleza sababu gani.

Monique na Li

“Yesu alitia moyo wanafunzi wake ‘wahesabie garama.’ Kwa hiyo, nilijiuliza hivi: ‘Je, niko na feza za kunisaidia kuhama? Je, nitaweza kujitimizia mahitaji yangu katika inchi hiyo bila kutumia wakati mwingi katika kazi ya kimwili?’” Anaongeza hivi: “Bila kukawia, nilitambua kama sikukuwa na feza za kutosha ili kuhamia upande huo mwingine wa dunia.” Sasa, namna gani aliweza kuhama?​—Lu. 14:28.

Monique anasema hivi: “Siku moja mukubwa wangu wa kazi aliniomba tuonane. Nilikuwa na wasiwasi, kwa sababu niliwaza kama atanifukuza kwenye kazi. Lakini, kuliko kunifukuza, mukubwa wangu wa kazi alinishukuru kwa ajili ya kazi yangu ya muzuri. Kisha aliniambia kama alifanya mipango ili nipate matabishi. Feza hizo za matabishi zilikuwa kiasi cha feza zenye nilikuwa nazo lazima!”

Monique anatumikia katika Myanmar tangu Mwezi wa 12, 2014. Anajisikia namna gani kuhusu kutumikia mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri? Anasema hivi: “Kuwa hapa kunaniletea furaha sana. Ninaongoza mafunzo tatu ya Biblia. Mumoja kati ya wanafunzi wangu iko na miaka 67. Sikuzote ananisalimia kwa sura ya kicheko na kunikumbatia sana. Alilia wakati alijifunza kama jina la Mungu ni Yehova. Alisema hivi: ‘Katika maisha yangu, hii ndiyo mara ya kwanza ninasikia kama jina la Mungu ni Yehova. Niko mukubwa sana kwako, lakini umenifundisha jambo la maana sana lenye singeweza kujua.’ Kwa kweli, mimi pia nilianza kulia. Mambo kama hayo yanafanya maisha ya kutumikia mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri yakuwe yenye furaha sana.” Hivi majuzi, Monique alipata pendeleo la kusoma Masomo kwa Ajili ya Waeneza-Injili wa Ufalme.

Kuko jambo lingine lenye lilichochea ndugu na dada fulani wahamie Myanmar. Ni habari kuhusu inchi hiyo yenye ilizungumuziwa katika Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova cha 2013. Dada mumoja mwenye kuwa na miaka zaidi ya 30 mwenye kuitwa Li tayari alikuwa anaishi katika Asia ya Kusini-Mashariki. Alikuwa na kazi yenye kuchukua wakati wote, lakini Kitabu cha Mwaka kilimuchochea afikirie kutumikia katika Myanmar. Anasema hivi: “Katika mwaka wa 2014 wakati nilihuzuria mukusanyiko wa pekee katika Yangon, nilikutana na bibi mumoja na bwana yake wenye walihamia katika Myanmar ili kusaidia kuhubiria watu wenye kuzungumuza Kichina. Kwa sababu ninazungumuza Kichina, niliamua kuhamia Myanmar ili kusaidia kikundi cha luga ya Kichina huko. Nilijiunga na Monique, na tulihamia Mandalay. Yehova alitubariki. Tulipata kwenye masomo moja kazi ya kufundisha yenye haikamate wakati wote, na tulipata nyumba ya kupanga karibu na masomo hayo. Hata kama kuko joto mingi na magumu fulani, ninafurahia utumishi wangu hapa. Watu katika Myanmar wanaishi maisha mepesi, lakini wako na adabu na wako tayari kutumia wakati wao ili kusikiliza habari njema. Inapendeza sana kuona namna Yehova iko anafanya kazi iende haraka. Ninaamini kabisa kama kuwa kwangu hapa Mandalay ni mapenzi ya Yehova.”

YEHOVA ANASIKILIZA SALA

Wahubiri wengi wenye kutumikia mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri wamejionea kama sala iko na nguvu. Tuzungumuzie Jumpei, mwenye kuwa na miaka 37, na bibi yake, Nao, mwenye kuwa na miaka 35. Tayari walikuwa wanatumikia katika kutaniko la luga ya ishara huko Japani. Sababu gani walihamia Myanmar? Jumpei anasema hivi: “Mimi na bibi yangu tayari tulikuwa na muradi wa kutumikia mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri katika inchi ya kigeni. Ndugu mumoja wa kutaniko letu la luga ya ishara katika Japani alihamia Myanmar. Katika Mwezi wa 5, 2010, sisi pia tulihama hata kama feza zenye tulikuwa tumechunga zilikuwa kidogo. Ndugu na dada katika Myanmar walitukaribisha kwa uchangamufu!” Anajisikia namna gani juu ya kuhubiria watu wenye kuzungumuza luga ya ishara katika Myanmar? Anasema hivi: “Watu wanapendezwa sana. Wakati tunawaonyesha video za luga ya ishara, wasikilizaji wetu wenye kuzungumuza luga ya ishara wanashangaa sana. Tuko wenye furaha sana kwa sababu tulikamata uamuzi huo wa kumutumikia Yehova hapa!”

Nao na Jumpei

Namna gani Jumpei na Nao wamepata feza ili kujitimizia mahitaji yao ya kimwili? Jumpei anasema hivi: “Kisha miaka tatu, tulikuwa tumetumia karibu feza zote zenye tulikuwa tumeweka, na hatukukuwa na feza za kutosha ili kulipia nyumba mwaka wenye kufuata. Mimi na bibi yangu tulisali sana. Bila kutazamia, tulipokea barua kutoka kwenye biro ya tawi yenye ilituomba tukuwe mapainia wa pekee kwa muda fulani! Tulimutegemea Yehova, na tuliona kama hakutuacha. Ametuhangaikia katika kila njia.” Hivi majuzi, Jumpei na Nao walisoma pia Masomo kwa Ajili ya Waeneza-Injili wa Ufalme.

YEHOVA ANACHOCHEA WATU WENGI

Ni nini ilichochea Simone, ndugu mwenye kuwa na miaka 43, muzaliwa wa inchi ya Italia, na bibi yake, Anna, dada mwenye kuwa na miaka 37, muzaliwa wa inchi ya Nouvelle Zélande, wahamie Myanmar? Anna anajibu hivi: “Ilikuwa habari juu ya Myanmar yenye ilikuwa katika Kitabu cha Mwaka cha 2013!” Simone anasema hivi: “Ni pendeleo kubwa kuwa katika Myanmar. Hapa maisha yako mepesi sana na ninaweza kupitisha wakati mwingi katika kazi ya Yehova. Inafurahisha kuona namna Yehova anatuhangaikia wakati tunatumikia katika eneo lenye kuwa na lazima kubwa ya wahubiri.” (Zb. 121:5) Anna anasema hivi: “Niko mwenye furaha sana kuliko wakati mwingine wowote. Tunaishi maisha mepesi. Ninapitisha wakati mwingi pamoja na bwana yangu, na tumekaribiana sana. Pia, tumepata marafiki wapya wazuri. Watu hawana ubaguzi kuelekea Mashahidi wa Yehova, na wanapendezwa sana!” Katika njia gani?

Simone na Anna

Anna anasema hivi: “Siku moja, nilihubiria kijana mwanamuke kwenye soko mwenye alikuwa anasoma masomo ya juu na nikafanya mipango ili kumurudilia. Wakati nilimurudilia, alikuwa ameleta rafiki yake. Wakati wenye kufuata, alileta wengine fulani. Kisha, akaleta wengine zaidi. Sasa, niko najifunza na tano kati yao.” Simone anasema hivi: “Watu katika eneo wako wenye urafiki na wanataka kujua mambo mengi. Wengi wanapendezwa. Hatuna kabisa wakati wa kutosha ili kusaidia watu wote wenye kupendezwa.”

Sachio na Mizuho

Lakini, tuseme nini juu ya hatua zenye kufaa zenye watu walipaswa kufanya ili kukamata uamuzi wa kuhamia Myanmar? Mizuho, mwenye alitoka Japani, anasema hivi: “Sikuzote mimi na bwana yangu, Sachio, tulikuwa tunapenda kutumikia katika inchi yenye kuwa na lazima kubwa ya wahubiri, lakini tulikuwa tunajiuliza ikiwa tutatumikia wapi. Kisha kusoma habari katika Kitabu cha Mwaka cha 2013 juu ya Myanmar, tuliguswa moyo sana na habari zenye kupendeza; kwa hiyo tulianza kufikiria ikiwa ingewezekana tutumikie katika Myanmar.” Sachio anaongeza hivi: “Tuliamua kutembelea kwa juma moja Yangon, muji mukubwa katika Myanmar, ili kupeleleza inchi kwa njia ya mufano. Matembezi hayo ya wakati mufupi yalitusaidia kuvumbua mambo yenye yalituhakikishia kama tunapaswa kuhamia hapa.”

UNAWEZA KUKUBALI MUALIKO?

Jane, Danica, Rodney, na Jordan

Rodney, na bibi yake, Jane, mwenye kuwa na miaka 52, wenye walitoka Australia, na Jordan, mutoto wao mwanaume, na Danica, mutoto wao mwanamuke, wametumikia katika Myanmar tangu mwaka wa 2010. Rodney anasema hivi: “Jambo lenye lilituchochea sana ni kuona kama watu walikuwa na njaa ya kiroho. Ninatia moyo kabisa familia zingine zijaribu kutumikia katika eneo lenye kuwa kama Myanmar.” Sababu gani? “Kufanya vile kumesaidia sana familia yetu katika hali ya kiroho! Vijana wengi wanahangaikia sana telefone zao, magari yao, kazi zao, na mambo mengine. Lakini, watoto wetu wanahangaikia sana kujifunza maneno ya mupya ya kutumikisha katika kazi ya kuhubiri. Wanajikaza kujifunza namna ya kufikiri pamoja na watu wenye hawajue Biblia na namna ya kujibu katika mikutano ya kutaniko, na wanafanya kwa bidii mambo mengine mengi ya kiroho yenye kufurahisha.”

Oliver na Anna

Oliver, ndugu mwenye kuwa na miaka 37, mwenye alitoka katika inchi ya Amerika, anaeleza sababu gani anatia wengine moyo wafanye aina hiyo ya utumishi. Anasema hivi: “Kuacha mambo na hali zenye nimezoea ili kuenda kumutumikia Yehova mahali pengine kumeniletea faida nyingi. Kuhamia mbali na nyumbani kumenisaidia nimutegemee Yehova zaidi hata nijikute katika hali gani. Kutumika pamoja na watu wenye sikujuana nao zamani lakini wenye kuwa na imani kama yangu, kumenisaidia kuona kama hakuna kitu cha maana zaidi katika ulimwengu chenye tunaweza kulinganisha na Ufalme wa Mungu.” Leo, Oliver na bibi yake, Anna, wanaendelea kuhubiria kwa bidii watu wenye kuzungumuza luga ya Kichina.

Trazel

Trazel, dada mwenye kuwa na miaka 52 mwenye alitoka Australia, ametumikia katika Myanmar tangu mwaka wa 2004. Anasema hivi: “Ninatia moyo sana wale wenye hali zao zinawaruhusu watumikie mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri. Nimejionea kwamba, kama uko na nia ya kutumika, Yehova anabariki bidii yako. Sikuwazia hata kidogo kama ningekuwa na maisha kama haya. Ndiyo maisha ya muzuri na yenye kufurahisha kabisa yenye nilipenda kuwa nayo.”

Maneno hayo yenye kutoka moyoni ya watu wenye kutumikia katika Myanmar, kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri, yakutie basi moyo ufikirie kusaidia watu wenye mioyo ya muzuri katika maeneo yenye hayajahubiriwa. Ndiyo, wale wenye walihamia Myanmar, wanatoa mualiko huu: “Tafazali, mukuje Myanmar na mutusaidie!”