Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | UTAKUBALI ZAWADI YA MUNGU YENYE KUWA KUBWA ZAIDI?

Zawadi Yenye Kuwa Tofauti na Zingine

Zawadi Yenye Kuwa Tofauti na Zingine

KIFAA fulani cha kuchonga kalamu chenye kuwa na umbo la mashua chenye Jordan anakamata kinaonekana kuwa hakina maana. Lakini, kiko kati ya vitu vyake vya maana sana. Jordan anaeleza hivi: “Russell, rafiki mwenye kuzeeka wa familia yetu, alinipatia kifaa hicho wakati nilikuwa mutoto.” Kisha kifo cha Russell, Jordan aliambiwa kwamba Russell alifanya mambo mengi katika maisha ya wazazi wake na katika maisha ya baba ya mama yake, alikuwa anawatia moyo wakati wa magumu. Jordan anasema hivi: “Kwa kuwa sasa nimejifunza mengi zaidi kuhusu Russell, ninaona zawadi hii ndogo kuwa ya maana sana kuliko zamani.”

Kama vile mufano wa Jordan unaonyesha, watu fulani wanaweza kuona kwamba zawadi fulani haina maana ao iko na maana kidogo. Lakini, kwa mutu mwenye shukrani ambaye alipokea zawadi hiyo, inaweza kuwa ya maana sana. Biblia inazungumuzia zawadi ya maana zaidi kwa kutumia maneno haya yenye kujulikana sana: ‘Kwa maana Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akamutoa Mwana wake muzaliwa-pekee, ili kila mutu anayemwamini asiangamizwe bali akuwe na uzima wa milele.’—Yohana 3:16.

Mutu mwenye kupokea zawadi hiyo anaweza kupata uzima wa milele. Kunaweza kuwa zawadi ingine ya maana zaidi kuliko zawadi hiyo? Hata kama watu fulani hawatambue faida ya zawadi hiyo, Wakristo wa kweli wanaiona kuwa ya ‘samani.’ (Zaburi 49:8; 1Petro 1:18, 19) Sababu gani Mungu alitoa maisha ya Mwana wake ili kuwa zawadi kwa ulimwengu?

Mutume Paulo anaeleza sababu hiyo katika maneno haya: ‘Kupitia mutu mumoja zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi, na hivyo kifo kikaenea kwa watu wote.’ (Waroma 5:12) Adamu, mutu wa kwanza, alifanya zambi kimakusudi kwa kukosa kumutii Mungu, kwa hiyo, alipata hukumu ya kifo. Kupitia Adamu, kifo kilienea kwa wazao wake wote, ni kusema, wanadamu wote.

‘Mushahara ambao zambi hulipa ni kifo, lakini zawadi ambayo Mungu hutoa ni uzima wa milele kupitia Kristo Yesu Bwana wetu.’ (Waroma 6:23) Ili kukomboa wanadamu kutoka katika hukumu ya kifo, Mungu alituma Mwana wake, Yesu Kristo, katika dunia ili atoe uzima wake mukamilifu kwa ajili ya ulimwengu. Kwa musingi wa zabihu hiyo ya ukombozi yenye kuitwa pia “fidia,” wale wote wenye kuonyesha imani katika Yesu watapata uzima wa milele.—Waroma 3:24.

Kuhusu baraka zote zenye Mungu anatolea waabudu wake kupitia Yesu Kristo, mutume Paulo anasema hivi: “Mungu apewe shukrani kwa ajili ya zawadi yake ya bure isiyoelezeka.” (2 Wakorintho 9:15) Kwa kweli, zabihu ya ukombozi ni zawadi ya maana sana kiasi cha kwamba hatuwezi kupata maneno ya kuifasiria. Kati ya zawadi nzuri zenye Mungu ametolea wanadamu, sababu gani zabihu ya ukombozi ni zawadi ya pekee? Katika njia gani ni tofauti na zawadi zingine zote za Mungu? * Na inapaswa kutuchochea kufanya nini? Tunakuomba usome majibu yenye Biblia inatoa kwa maulizo hayo katika habari mbili zenye kufuata.

^ fu. 8 Kwa kupenda, Yesu “aliitoa nafsi [ao, uzima] yake kwa ajili yetu.” (1 Yohana 3:16) Lakini, kwa kuwa zabihu hiyo ilikuwa katika kusudi la Mungu, habari hii na habari mbili zenye kufuata zinakazia daraka la Mungu ambaye ni Mutoaji wa zabihu ya ukombozi.