Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Ni wanani njo watafufuliwa ku dunia, na watapata ufufuo gani?

Ona namna Biblia inajibia ile maulizo.

Matendo 24:15 inatuambia kama kutakuwa “ufufuo wa wenye haki na wenye hawako wenye haki.” Wenye haki ni wale wenye mbele wakufe walikuwa natii Mungu. Njo maana majina yao iliandikwa mu kitabu ya uzima. (Mal. 3:16) Wale wenye hawako wenye haki ni wale wenye walikufa bila kupata kabisa nafasi ya kujifunza juu ya Yehova. Njo maana majina yao haiko mu kitabu ya uzima.

Yohana 5:28, 29 inazungumuzia pia vile vikundi mbili vyenye kutajwa mu Matendo 24:15. Yesu alisema kama “wale wenye walitenda mambo ya muzuri” watafufuliwa “kwenye ufufuo wa uzima, na wale wenye walizoea kutenda mambo maovu kwenye ufufuo wa hukumu.” Wenye haki walifanya mambo ya muzuri mbele ya kufa. Watapata ufufuo wa uzima juu majina yao ingali naandikwa mu kitabu ya uzima. Lakini, wale wenye hawako wenye haki walifanya mambo ya mubaya mbele wakufe. Watapata ufufuo wa hukumu. Majina yao haiyaandikwa mu kitabu ya uzima. Kwa hiyo, watakuwa mu kipindi fulani ya hukumu ao ya kuchunguzwa. Mu ile kipindi, watapata nafasi ya kujifunza juu ya Yehova na majina yao itaandikwa mu kitabu ya uzima.

Ufunuo 20:12, 13 inafasiria kama itaomba wale wote wenye kufufuliwa watii “mambo yenye kuandikwa katika vile vitabu vya kukunjwa,” ni kusema, sheria za mupya zenye Mungu atatupatia mu dunia mupya. Wale wenye hawatatii wataharibiwa.​—Isa. 65:20.

Danieli 12:2 inasema kama watu fulani wenye kulala usingizi katika kifo watalamuka “kwenye uzima wa milele na wengine kwenye haya na zarau ya milele.” Hii andiko inazungumuzia hukumu ya mwisho ya wale wenye watafufuliwa, ni kusema, watapata “uzima wa milele” ao “zarau ya milele.” Kwa hiyo, ku mwisho wa miaka 1000, wamoja watapata uzima wa milele, na wengine wataharibiwa milele.​—Ufu. 20:15; 21:3, 4.

Tukamate mufano. Hali ya vile vikundi mbili vya wale wenye watafufuliwa inaweza kulinganishwa na hali ya wale wenye wanapenda kuishi mu inchi ingine. Wenye haki wako sawa vile wale wenye wanapewa viza ya wafanyakazi ao viza ya wakaaji yenye inawapatia utambulisho na uhuru fulani. Lakini, wenye hawako wenye haki wako sawa vile watu wenye wanapewa viza ya muda ao viza ya wageni. Wote wanapaswa kuheshimia na kutii sheria za inchi juu waendelee kuruhusiwa kubakia mu ile inchi. Vilevile, wale wenye hawako wenye haki wenye watafufuliwa watakuwa na lazima ya kutii sheria za Yehova na kuonyesha kama wako wenye haki juu waendelee kuishi mu paradiso. Hata ikuwe watu walipewa viza gani mbele ya kuhamia mu inchi ingine, kisha wakati fulani wamoja wanaweza kukubaliwa kuwa raia wa ile inchi, na wengine wanaweza kufukuzwa. Ni mwenendo wa mutu mu ile inchi njo utafanya aruhusiwe kubakia mu ile inchi ao hapana. Vilevile, ni uaminifu na mwenendo wa wale wote wenye watafufuliwa njo utafanya waruhusiwe kuendelea kubakia mu dunia mupya.

Yehova ni Mungu mwenye upendo, lakini pia ni Mungu wa haki. (Kum. 32:4; Zb. 33:5) Ataonyesha upendo wake kwa kufufua wenye haki na wenye hawako wenye haki. Lakini, atatazamia wote watii kanuni zake za mema na mabaya. Ni wale tu wenye wanamupenda na kutii kanuni zake njo wataruhusiwa kuendelea kuishi mu dunia mupya.