Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mushiriki Mupya wa Baraza Linaloongoza

Mushiriki Mupya wa Baraza Linaloongoza

Siku ya Tatu asubuhi, tarehe 5 Mwezi wa 9, 2012, tangazo lilitolewa kwa Wanabeteli wa États-Unis na Canada kwamba mushiriki mupya ameongezwa kwenye Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova. Yeye ni Ndugu Mark Sanderson, na alianza kutumika kwenye Baraza Linaloongoza tarehe 1 Mwezi wa 9, 2012.

Ndugu Sanderson alikomalia katika muji wa San Diego, California, États-Unis. Alilelewa na wazazi Mashahidi na alibatizwa tarehe 9 Mwezi wa 2, 1975. Alianza kazi ya upainia katika Saskatchewan, Canada, tarehe 1 Mwezi wa 9, 1983. Katika Mwezi wa 12, 1990, alimaliza Shule ya Mazoezi ya Kihuduma (inayoitwa sasa, Masomo ya Biblia kwa Ajili ya Ndugu Wasio na Bibi) huko États-Unis. Katika Mwezi wa 4, 1991, Ndugu Sanderson alitumwa kufanya kazi ya upainia wa pekee katika kisiwa cha Terre-Neuve, Canada. Kisha kufanya kazi ya mwangalizi wa badala, alialikwa kwenye Beteli ya Canada katika Mwezi wa 2, 1997. Katika Mwezi wa 11, 2000, alitumwa kwenye Beteli ya États-Unis, ambako alitumika katika Biro ya Huduma za Habari za Kihospitali na baadaye alitumika katika Biro ya Utumishi.

Katika Mwezi wa 9, 2008, Ndugu Sanderson alialikwa kwenye Masomo ya Washiriki wa Halmashauri ya Tawi na baadaye alitumika katika Halmashauri ya Tawi ya Philippines. Katika Mwezi wa 9, 2010, aliitwa tena kwenye Beteli ya États-Unis, ambako alitumika akiwa musaidizi katika Halmashauri Utumishi ya Baraza Linaloongoza.