Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAZUNGUMUZO YA BIBLIA PAMOJA NA JIRANI

Je, Mungu Anahangaika juu ya Mateso Yetu?

Je, Mungu Anahangaika juu ya Mateso Yetu?

Habari inayofuata ni mufano wa mazungumuzo ambayo Shahidi wa Yehova fulani anaweza kuwa nayo pamoja na jirani yake. Kwa mufano, Shahidi fulani anayeitwa Micheline anamukuta mwanamuke anayeitwa Sophia nyumbani kwake.

SABABU GANI MUNGU ANAACHA JAMBO HILI LITOKEE?

Micheline: Leo ninamutolea kila mutu trakti hii katika eneo hili. Ina kichwa cha habari Je, Ungependa Kujua Kweli? Kamata kopi yako.

Sophia: Je, inahusu dini?

Micheline: Ndiyo. Ona maulizo sita ambayo yanaonyeshwa kwenye ukurasa wa kwanza. Kati ya maulizo haya ni ulizo gani—

Sophia: Achia pale. Utapoteza wakati wako kuzungumuza na mimi.

Micheline: Sababu gani unasema hivyo?

Sophia: Kwa kweli, sijue hata kama kuna Mungu.

Micheline: Sawa, unafanya vizuri kwa kuniambia mambo waziwazi. Nikuulize kidogo, umekuwa na maoni hayo sikuzote?

Sophia: Hapana, nilipokuwa ninakomaa, nilikuwa ninaenda kwenye kanisa. Lakini niliacha kuenda huko kumepita miaka mingi.

Micheline: Ah, ninaelewa. Lakini, acha nikuambie jina langu. Jina langu Micheline.

Sophia: Na mimi jina langu Sophia.

Micheline: Ninafurahi kukujua, Sophia.

Sophia: Na mimi pia.

Micheline: Sikuja kukulazimisha ukubali imani yangu, Sophia. Hata hivyo, ningependa kujua, je, kuna jambo fulani kabisa ambalo lilikufanya uwe na mashaka kwamba kuna Mungu?

Sophia: Ndiyo. Mama yangu alifanya aksida ya motokari kumepita miaka 17.

Micheline: Ninasikitika kusikia hivyo. Je, aliumia?

Sophia: Ndiyo, aliumia na tangu wakati huo amekuwa mwenye kupooza.

Micheline: Oh, hilo ni jambo lenye kuhuzunisha sana. Unapaswa kuwa mwenye kuvurugika kabisa.

Sophia: Ndiyo, ninavurugika kwelikweli. Ndiyo maana ninajiuliza, ikiwa kuna Mungu, sababu gani aliacha jambo hilo litokee? Sababu gani Mungu anaacha tuteseke hivi?

JE, NI VIBAYA MUTU KUULIZA SABABU GANI MUNGU ANAACHA WATU WATESEKE?

Micheline: Namna unavyojisikia moyoni inaeleweka na maulizo yako yote yanaeleweka pia. Wakati tunateseka, ni kawaida kujiuliza sababu gani. Kwa kweli, hata wanaume na wanawake fulani waaminifu wa zamani walijiuliza hivyo!

Sophia: Ni kweli?

Micheline: Ndiyo. Je, utafurahi nikuonyeshe mufano mumoja katika Biblia?

Sophia: Ndiyo nitafurahi.

Micheline: Ona mambo ambayo nabii mwaminifu Habakuki alimuuliza Mungu, kama inavyoandikwa katika Habakuki, sura ya 1, mustari wa 2 na wa 3: ‘Ee Yehova, nililie musaada mupaka wakati gani, nawe usisikie? Nitakuomba musaada kutokana na jeuri mupaka wakati gani, nawe usiokoe? Kwa nini unanionyesha jambo lenye kuzuru?’ Je, maulizo hayo yanafanana na yale unayojiuliza?

Sophia: Ndiyo.

Micheline: Mungu hakumukemea hata kidogo nabii Habakuki kwa kumuuliza maulizo hayo, wala hakumuambia kwamba ana imani ndogo.

Sophia: Hilo linapendeza.

YEHOVA ANACHUKIA MATESO

Micheline: Biblia inafundisha kwamba Mungu anaona namna tunavyoteseka na kwamba anahangaika juu ya mateso yetu.

Sophia: Unataka kusema nini?

Micheline: Acha nikuonyeshe mufano mumoja katika andiko la Kutoka 3:7. Tafazali, unaweza kusoma andiko hilo?

Sophia: Sawa. Linasema hivi: “Naye Yehova akaongezea: ‘Pasipo shaka nimeyaona mateso ya watu wangu walio Misri, nami nimesikia kilio chao kwa sababu ya wale wanaowalazimisha kufanya kazi; kwa sababu nayajua vizuri maumivu waliyo nayo.’”

Micheline: Aksanti. Kupatana na andiko hilo, je, Mungu anaona wakati watu wake wanateseka?

Sophia: Ndiyo, inaonekana ni hivyo.

Micheline: Na hatuwezi kusema kwamba hajue mambo yote yanayotokea. Angalia tena sehemu ya mwisho ya andiko hilo. Mungu alisema hivi: “Nayajua vizuri maumivu waliyo nayo.” Je, unasikia hayo kuwa maneno ya Mungu ambaye hatuhangaikie ao aliye mbali sana na sisi?

Sophia: Hapana, si hivyo kabisa.

Micheline: Bila shaka, Mungu haone tu mateso yetu, lakini pia anahuzunika wakati tunateseka.

Sophia: Ni kweli.

Micheline: Tukiwa na jambo hilo katika akili, acha tusome kuhusu wakati mwengine ambapo watu wa Mungu waliteseka. Habari hiyo inapatikana katika andiko la Isaya 63:9. Sehemu ya kwanza ya andiko hilo inasema hivi: ‘Wakati wa taabu zao zote hilo lilimutaabisha.’ Je, hauone kwamba Mungu alihangaika juu ya mateso ya watu wake?

Sophia: Ndiyo, inaonekana hivyo.

Micheline: Sophia, ni kweli kwamba Mungu anatuhangaikia sana, na anachukia wakati anatuona tunateseka. Wakati tunateseka, Mungu anahuzunika.

SABABU GANI MUNGU ANAKAWIA KUMALIZA MATESO?

Micheline: Mbele niende, nina jambo lingine moja ningependa tuzungumuzie.

Sophia: Sawa.

Micheline: Tuone mambo ambayo Biblia inatufundisha kuhusu nguvu za Mungu. Andiko ambalo ninafikiria ni Yeremia 10:12. Tafazali, ungependa kusoma andiko hilo?

Sophia: Bila shaka. Linasema hivi: ‘Yeye ndiye Mutengenezaji wa dunia kwa nguvu zake, Yeye anayeifanya imara inchi yenye kuzaa kwa hekima yake, na Yeye aliyezitandaza mbingu kwa uelewaji wake.’

Micheline: Aksanti. Acha tufikiri kidogo juu ya andiko hilo. Je, Mungu alihitaji nguvu nyingi ili kuumba ulimwengu wote na kila kitu kilicho ndani ya ulimwengu?

Sophia: Bila shaka.

Micheline: Sasa, ikiwa Mungu ana nguvu za kuumba kila kitu tunachoona, je, hatuwezi kutazamia kwamba ana pia nguvu za kumaliza mateso yetu?

Sophia: Ndiyo.

Micheline: Fikiri tena juu ya mama yako. Sababu gani unahuzunika wakati unamuona anateseka?

Sophia: Ni kwa sababu ninamupenda. Yeye ni mama yangu.

Micheline: Na kama ungekuwa na nguvu ya kumuponyesha leo, ungefanya hivyo?

Sophia: Bila shaka.

Micheline: Fikiria maana ya jambo hilo. Biblia inafundisha kwamba Mungu anaona mateso yetu, anahangaika juu ya mateso yetu, na ana nguvu nyingi sana. Je, unaweza kuwazia namna Mungu anavyojizuia sana ili asichukue hatua na kumaliza mateso yetu mara moja?

Sophia: Sijafikiria jambo hilo kwa njia hiyo.

Micheline: Je, inaweza kuwa kwamba ana sababu nzuri ya kukosa kuchukua hatua ili kumaliza mateso yetu? *

Sophia: Hmm, ninafikiri anapaswa kuwa na sababu nzuri.

Micheline: Ninasikia telefone yako inalia, kwa hiyo nitarudia wakati mwengine ili tuzungumuzie zaidi habari hii.

Sophia: Aksanti. Nitafurahi sana. *

Je, una ulizo fulani juu ya habari za Biblia ambalo umekwisha kujiuliza? Je, unapenda kujua mengi juu ya mambo ambayo Mashahidi wa Yehova wanaamini ao juu ya mambo fulani wanayofanya? Ikiwa jibu ni ndiyo, usisite kuuliza ulizo hilo wakati utakutana na Shahidi wa Yehova. Atafurahi kuzungumuzia mambo hayo pamoja na wewe.

^ Ili kupata habari zingine, soma sura ya 11 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

^ Habari inayofuata ya mufululizo huu itazungumuzia sababu gani Mungu anaacha watu wateseke.