Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | LIES THAT MAKE GOD SEEM UNLOVABLE

Kweli Inaweza Kukuweka Huru

Kweli Inaweza Kukuweka Huru

Siku moja, huko Yerusalemu, Yesu alikuwa anazungumuza juu ya Baba yake, Yehova, na alionyesha waziwazi makosa ya viongozi wa dini za uongo za wakati wake. (Yohana 8:12-30) Mambo ambayo alisema wakati huo yanatufundisha namna ya kuchunguza mafundisho juu ya Mungu yanayopendwa na watu wengi leo. Yesu alisema hivi: ‘Mukikaa katika neno langu, ninyi kwa kweli ni wanafunzi wangu, nanyi mutaijua kweli, nayo kweli itawaweka ninyi huru.’​—Yohana 8:31, 32.

‘Mukikaa katika neno langu.’ Hapa Yesu anatuonyesha namna tunaweza kujua ikiwa mafundisho ya kidini ni ya “kweli.” Unaposikia jambo fulani linasemwa juu ya Mungu, ujiulize, ‘Jambo hilo linapatana na maneno ya Yesu na sehemu zingine za Maandiko Matakatifu?’ Uige wale ambao walisikia mafundisho ya mutume Paulo na ambao walikuwa “wakiyachunguza Maandiko kwa uangalifu kila siku ili kuona kama mambo hayo ndivyo yalivyo.”​—Matendo 17:11.

Marco, Rosa, na Raymonde, ambao walitajwa wote katika habari ya kwanza ya gazeti hili, walichunguza kwa uangalifu mafundisho ya dini zao kwa kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Walisema nini juu ya mambo waliyojifunza?

Marco: “Mwalimu wetu aliyetufundisha Biblia alitumia Maandiko ili kujibu kila ulizo ambalo mimi na bibi yangu tuliuliza. Mimi na bibi yangu tulianza kumupenda Yehova, na uhusiano kati yangu na bibi yangu ukakuwa wenye nguvu sana!”

Rosa: “Kwanza, nilifikiri kwamba Biblia ni kitabu ambacho kina mawazo tu ya wanadamu juu ya namna Mungu alivyo. Hata hivyo, polepole, nilipata majibu ya Biblia kwa maulizo yangu. Sasa, ninamuona Yehova kuwa mutu kwelikweli. Yeye ni Mutu ambaye ninaweza kutumainia.”

Raymonde: “Nilimuomba Mungu anisaidie kujifunza juu yake. Muda kidogo kisha hapo, mimi na bwana yangu tulianza kujifunza Biblia. Mwishowe, tulijua kweli kumuhusu Yehova! Tulifurahi sana kutambua Yehova ni Mungu wa aina gani.”

Biblia haionyeshe tu mafundisho ya uongo juu ya Mungu; inaonyesha pia kweli kuhusu sifa zake zenye kuvutia. Biblia ni Neno la Mungu ambalo liliongozwa na roho yake, inatusaidia ‘tuyajue mambo ambayo Mungu ametupa sisi kwa fazili,’ ni kusema, kuelewa kweli kumuhusu yeye na makusudi yake. (1 Wakorintho 2:12) Unaweza kuchunguza wewe mwenyewe namna Biblia inavyojibia maulizo ya maana ambayo watu wanauliza kwa ukawaida juu ya Mungu, makusudi yake, na wakati wetu unaokuja. Soma majibu ya maulizo fulani kati ya maulizo hayo kwa kufungua kichwa http://www.ps8318.com/en/bible-teachings/questions?wtlocale=ZS

“Mafundisho ya Biblia > Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa” kwenye adresi yetu ya Internete www.ps8318.com. Unaweza pia kuomba funzo la Biblia kupitia adresi yetu ya Internete ao kwa kutafuta Shahidi mumoja wa Yehova. Tuna uhakika kwamba ukifanya hivyo, utaona kuwa ni vyepesi zaidi kumupenda Mungu kuliko ulivyowazia.