Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 BIBLIA INABADILISHA MAISHA YA WATU

Nilikuwa Mwenye Kujifikiria Sana Katika Maisha

Nilikuwa Mwenye Kujifikiria Sana Katika Maisha
  • ALIZALIWA MWAKA WA: 1951

  • INCHI: UJERUMANI

  • ALIKUWA: MWENYE KIBURI NA MWENYE KUJITEGEMEA

MAISHA YANGU YA ZAMANI:

Miaka kidogo ya kwanza katika maisha yangu, familia yetu iliishi karibu na Leipzig, Mashariki mwa Ujerumani, haikukuwa mbali sana na Jamuhuri ya Cheki na mipaka ya Polandi. Wakati nilikuwa na miaka sita, kazi ya baba yangu ilitufanya tuhamie katika inchi zingine mbali na kwetu, kwanza tulihamia katika inchi ya Brazil na kisha tulihamia katika inchi ya Ekwado Marekani (Équateur).

Wakati nilikuwa na miaka 14, nilitumwa kwenye masomo ya bweni (internat) katika inchi ya Ujerumani. Kwa sababu wazazi wangu walikuwa mbali sana katika Amerika ya Kusini, nilipaswa kujihangaikia mimi mwenyewe. Nilianza kujitegemea sana. Sikufikiria hata kidogo namna matendo yangu yangewaumiza wengine.

Wakati nilikuwa na miaka 17, wazazi wangu walirudia Ujerumani. Kwanza, niliishi nao nyumbani. Lakini kwa sababu ya roho yangu ya kujitegemea sikuweza kuishi chini ya mamlaka ya wazazi wangu. Wakati nilikuwa na miaka 18, niliondoka nyumbani.

Niliendelea kukosa utulivu, nikitafuta kusudi la maisha. Kisha kuchunguza maisha ya aina mbalimbali na vikundi, nilipata uhakika kwamba namna nzuri ya kutumia maisha yangu ni kutembea katika dunia hii nzuri mbele watu waiharibishe.

Niliondoka Ujerumani, na nikaelekea Afrika kwa kutumia pikipiki. Lakini, kisha muda mufupi, nilirudia Ulaya ili kutengenezesha pikipiki yangu. Muda kidogo kisha hapo, nilijikuta kwenye sehemu ya muchanga pembeni ya bahari katika inchi ya Ureno (Portugal). Niliamua kuacha kusafiri kwa pikipiki na kuanza kusafiri kwa mashua.

Nilijiunga na kikundi cha vijana waliokuwa wanapanga kusafiri kwa mashua kuzunguka Bahari ya Atlantiki. Kati ya vijana hao nilikutana na Laurie, aliyekuja kuwa bibi yangu. Kwanza, tulisafiri mupaka visiwa vya Karibea. Kisha, tulibakia kwa muda mufupi katika Porto Rico, na baadaye tukarudia Ulaya. Tulitumaini kupata mashua yenye kuwa na motere ambayo tungefanya kuwa nyumba yetu. Lakini kisha kutafuta kwa miezi tatu tu, mupango wetu ulivunjwa. Nilikamatwa kwa nguvu na maaskari wa Ujerumani.

Nilimaliza miezi 15 katika jeshi la Ujerumani linalopigana likiwa katika maji. Katika miezi hiyo, mimi na Laurie tulioana na tukajitayarisha kuendelea na maisha yetu ya kusafiri. Muda mufupi mbele ya kuanza kutumika katika jeshi, tulinunua sehemu ya inje ya mashua ndogo ya kuokoa watu. Wakati nilikuwa ninatumika katika jeshi, tulibadilisha pole kwa pole sehemu hiyo kuwa mashua ndogo. Tulipanga kuishi katika mashua hiyo na kuendelea kusafiri katika dunia yetu hii nzuri. Wakati huo, kisha kuacha kazi yangu ya jeshi lakini mbele ya kumaliza kujenga mashua yetu, Mashahidi wa Yehova walitutembelea na tukaanza kujifunza nao Biblia.

BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU:

Kwanza, sikuona ulazima wa kufanya mabadiliko makubwa katika maisha yangu. Nilikuwa nimemuoa kisheria mwanamuke ambaye nilikuwa ninaishi naye, na nilikuwa nimeacha kuvuta tumbaku. (Waefeso 5:5) Kuhusu mupango wetu wa kusafiri katika dunia yote, nilifikiri kwamba kutumia maisha yetu ili kuangalia maajabu ya uumbaji wa Mungu haikukuwa kupoteza wakati.

Lakini, kwa kweli nilikuwa na lazima ya kufanya mabadiliko, zaidi sana katika namna yangu ya kuwa. Kwa sababu ya kuwa mwenye kiburi na mwenye kujitegemea, nilitumainia sana uwezo wangu na mambo nilikuwa ninatimiza. Nilikuwa mwenye kujifikiria sana katika maisha.

Siku moja, nilisoma Mahubiri ya Yesu ya Mulimani yenye kujulikana sana. (Mathayo, sura ya 5-7) Kwanza, nilivurugika sana niliposoma juu ya furaha ambayo Yesu alizungumuzia. Kwa mufano, Yesu alisema kwamba wenye furaha ni wale walio na njaa na kiu. (Mathayo 5:6) Nilijiuliza namna gani kuwa katika uhitaji kunaweza kumufanya mutu akuwe na furaha. Nilipoendelea kujifunza, nilifikia kutambua kwamba sisi wote tuko na uhitaji wa kiroho lakini tunapaswa kukubali kwa unyenyekevu uhitaji huo mbele ya kuutimiza. Ni kama vile Yesu alisema: “Wenye furaha ni wale wanaotambua uhitaji wao wa kiroho.”—Mathayo 5:3.

Kisha kuanza kujifunza Biblia katika inchi ya Ujerumani, mimi na Laurie tulihamia Ufaransa, na baadaye, tulihamia Italia. Tulikuta Mashahidi wa Yehova kila mahali tulienda. Nilipendezwa sana na umoja wao na upendo wa kweli ambao wanaonyeshana. Niliona kwamba Mashahidi wa Yehova ni familia kabisa ya ndugu katika dunia yote. (Yohana 13:34, 35) Kisha wakati fulani, mimi na Laurie tulibatizwa na kuwa Mashahidi wa Yehova.

Kisha kubatizwa, niliendelea kufanya mabadiliko katika namna yangu ya kuwa. Mimi na Laurie tuliamua kusafiri kwa mashua kwenye eneo la Afrika lenye kuwa pembeni-pembeni ya bahari na kisha katika bahari ya Atlantiki mupaka inchi ya Amerika. Wakati tulikuwa katika bahari hiyo, sisi wawili tu katika mashua hiyo ndogo tukizungukwa na maelfu ya kilometa ya maji, ndipo nilitambua kwamba sikukuwa kitu kabisa ninapolinganishwa na Muumbaji wetu mwenye utukufu. Nilikuwa na wakati mwingi kwa sababu sikukuwa na mambo mengi ya kufanya katika bahari, kwa hiyo nilitumia wakati mwingi katika kusoma Biblia. Niliguswa moyo na habari ya maisha ya Yesu duniani. Alikuwa mutu mukamilifu mwenye uwezo mbalimbali kupita kitu chochote ambacho ninaweza kuwazia, lakini hakuvutia uangalifu juu yake mwenyewe. Hakukuwa mwenye kujifikiria katika maisha lakini alifikiria Baba yake wa mbinguni.

Niliona kwamba nilikuwa na lazima ya kutia Ufalme wa Mungu penye nafasi ya kwanza katika maisha yangu

Nilipofikiri sana juu ya mufano wa Yesu, niliona kwamba nilikuwa na lazima ya kutia Ufalme wa Mungu penye nafasi ya kwanza katika maisha yangu kuliko kuupatanisha na mambo mbalimbali niliyotaka kufanya. (Mathayo 6:33) Wakati mimi na Laurie tulifika inchi kavu katika Amerika, tuliamua kukaa huko na kujitoa kabisa katika ibada yetu.

FAIDA AMBAYO NIMEPATA:

Maisha yangu ya zamani ya kujifikiria yalinifanya nikose uhakika juu ya mambo niliyokuwa ninafanya. Lakini, sasa, nimepata hekima ya kweli kabisa ya kuniongoza. (Isaya 48:17, 18) Nimepata pia kusudi katika maisha lenye sikukuwa nalo zamani, ni kusema, kumuabudu Mungu na kusaidia wengine wajifunze juu yake.

Kwa kutumia kanuni za Biblia, mimi na Laurie tumefanya ndoa yetu kuwa yenye nguvu. Pia, tumebarikiwa kwa kuzaa mutoto mwanamuke mwenye sura nzuri, anayemujua Yehova na kumupenda.

Siwezi kusema kwamba maisha yetu ya sasa ni mepesi sikuzote kama maisha yetu ya zamani ya kusafiri-safiri. Lakini kwa musaada wa Yehova, tumeamua kwamba hatutaacha hata siku moja kumutumikia Yehova na kumutumainia.—Methali 3:5, 6.