Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | KUSALI KUNALETA FAIDA FULANI?

Kuko Mutu Mwenye Kusikiliza Sala?

Kuko Mutu Mwenye Kusikiliza Sala?

Watu fulani wanaona kama kusali ni kupoteza tu wakati, na kama hakuna mutu mwenye kusikiliza sala. Wengine wamepima kusali lakini wanaona kama hawakupata jibu. Mutu mumoja, mwenye kuamini kama hakuna Mungu, alionyesha wazo lake juu ya namna Mungu anaweza kuwa, na akasali hivi: “Uzungumuze tu na mimi kwa sauti ya chini.” Lakini alisema kama Mungu alibakia “kimya kabisa.”

Hata hivyo, Biblia inatuhakikishia kama kuko Mungu mwenye kuishi kabisa anayesikiliza sala. Biblia inataja maneno haya yenye yaliambiwa watu fulani wa zamani: “Yeye [Mungu] hakika atakuonyesha kibali unapotoa sauti ya kilio chako; mara tu atakapokisikia kwa kweli atakujibu.” (Isaya 30:19) Andiko lingine la Biblia linasema hivi: “Sala ya wanyoofu ni furaha Kwake.”—Methali 15:8.

Yesu alisali kwa Baba yake, “naye akasikiwa vizuri.”—Waebrania 5:7

Tena, Biblia inazungumuzia mifano ya watu fulani wenye sala zao zilisikiwa. Andiko moja linasema kama Yesu alitoa ‘maombi . . . kwa Yule aliyekuwa na uwezo wa kumuokoa’ na kama “akasikiwa vizuri.” (Waebrania 5:7) Mifano mingine inaweza kupatikana katika Danieli 9:21 na 2 Mambo ya Nyakati 7:1.

Hata hivyo, sababu gani watu fulani wanaona kama sala zao hazijibiwe? Ili sala zetu zisikiwe, tunapaswa kusali tu kwa Mungu mwenye kutajwa katika Biblia, ni kusema Yehova, * hapana kwa mungu mwengine ao wazazi wetu wa zamani. Tena, Mungu anasema ‘tumuombe kulingana na mapenzi yake,’ ni kusema, juu ya mambo yenye anakubali. Ikiwa tunafanya hivyo, Mungu anatuhakikishia kama ‘anatusikiliza.’ (1 Yohana 5:14) Kwa hiyo, ili sala zetu zisikiwe, tunapaswa kujua Mungu mwenye kutajwa katika Biblia na kujifunza mapenzi yake.

Watu wengi wanahakikisha kama sala haiko tu desturi ya kidini, lakini Mungu anasikiliza sala na anazijibia. Isaac, wa inchi ya Kenya, anasema hivi: “Nilisali ili nipate musaada wa kuelewa Biblia. Kisha muda kidogo, mutu mumoja alinikaribia na kunitolea musaada wenye nilikuwa nao lazima.” Hilda, wa inchi ya Ufilipino, alitaka kuacha kuvuta tumbako. Kisha kushindwa mara nyingi, bwana yake alimushauria hivi: “Sababu gani usimuombe Mungu akusaidie?” Alifuata shauri hilo na anasema hivi: “Nilishangaa sana namna Mungu alinisaidia. Ilikuwa kama vile nilianza kupoteza hamu ya kuvuta tumbako. Niliacha kuvuta.”

Mungu anaweza kukusaidia katika mahangaiko yako yenye kupatana na mapenzi yake?

^ fu. 6 Biblia inaonyesha kama jina la Mungu ni Yehova.