Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

WIMBO 106

Tukuwe na Upendo

Tukuwe na Upendo

(1 Wakorinto 13:1-8)

  1. 1. Yehova utusaidie

    Kuwa na sifa kama zako.

    Zaidi ya yote upendo

    Wenye unatoka mu moyo.

    Na kama hatuna upendo,

    Imani yetu ni ya bure.

    Basi tuonyeshe upendo

    Kwa maneno na kwa matendo.

  2. 2. Upendo unatusukuma

    Kuwasaidia wengine,

    Na kusamehe ndugu zetu;

    Ni vile Yesu alisema.

    Upendo unavumilia

    Na unafunika makosa.

    Tutavumilia magumu

    Ikiwa tuko na upendo.