WIMBO 137
Wanamuke Wenye Imani
-
1. Hana, Maria, Sara, na wengine
Walikuwa na imani kabisa.
Walimuogopa sana Yehova.
Kuko tena wanamuke wengine
Wenye walimupenda Yehova,
Lakini Biblia haikuwataya.
-
2. Wale wanamuke walikuwa na
Upendo, uhodari, na imani,
Na sifa zingine za kuvutia.
Na leo tunaona dada zetu
Wenye kuwa washikamanifu.
Basi tuwaige, tutabarikiwa.
-
3. Wajane na mama na dada zetu,
Muko natumika kwa nguvu sana.
Muko wapole, tena watiifu.
Mujue, Yehova anawapenda.
Tunasali awasaidie
Ili musichoke, na mubarikiwe.
(Ona pia Flp. 4:3; 1 Ti. 2:9, 10; 1 Pe. 3:4, 5.)