WIMBO 8
Yehova Ni Kimbilio Yangu
-
1. Yehova Mungu wetu,
Uko kimbilio.
Tunakutegemea;
Hautatuacha.
Utalinda watu wako,
Hata nini itokee.
Mungu tusaidie,
Weye tu njo nguvu yetu.
-
2. Makumi ya maelfu
Wataanguka tu,
Lakini wenye haki
Wataendelea.
Hatupaswe kuogopa
Musiba ao mateso.
Mungu atatulinda
Chini ya mabawa yake.
-
3. Sitaogopa simba,
Nyoka na mutego.
Hata kukuwe giza,
Utaniokoa.
Baba, sitatetemeka,
Wala sitahangaika.
Yehova Mungu wangu,
Uko kimbilio yangu.
(Ona pia Zb. 97:10; 121:3, 5; Isa. 52:12.)