Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 47

Uko Tayari Kubatizwa?

Uko Tayari Kubatizwa?

Kujifunza Biblia kumekusaidia ujue mambo mingi juu ya Yehova. Na inawezekana umefanya mabadiliko fulani mu maisha yako juu utumikishe mambo yenye uko najifunza. Lakini, pengine kuko jambo fulani yenye ingali nakuzuia kujitoa kwa Yehova na kubatizwa. Mu hii somo, tutaona mambo fulani yenye inaweza kuzuia mutu kubatizwa, na tutaona unaweza kufanya nini juu isikuzuie.

1. Ni lazima ujue mambo mingi sana mbele ya kubatizwa?

Juu ubatizwe, unapaswa kuwa na “ujuzi wenye hauna makosa wa ile kweli.” (1 Timoteo 2:4) Ile haimaanishe kama mbele ubatizwe unapaswa kujua jibu ya kila ulizo yenye inahusu Biblia. Hata Wakristo wenye walibatizwa zamani wangali wanajifunza. (Wakolosai 1:9, 10) Lakini, unapaswa kuelewa mafundisho ya musingi ya Biblia. Wazee wa kutaniko watakusaidia ujue ikiwa unaelewa kabisa mafundisho ya musingi ya Biblia.

2. Unapaswa kufanya mambo gani mbele ubatizwe?

Mbele ubatizwe, unapaswa ‘kutubu na kugeuka.’ (Soma Matendo 3:19.) Ile inamaanisha kama unapaswa kuhuzunika sana juu ya zambi zenye ulifanyaka zamani, na kuomba Yehova akusamehe. Tena unapaswa kuepuka kabisa mambo yenye Yehova anachukia na kujikaza sana kufanya mambo yenye inamufurahisha. Zaidi ya ile, unapaswa kuanza kukusanyika na kuhubiri pamoja na kutaniko.

3. Juu ya nini haupaswe kuacha woga ikuzuie kubatizwa?

Watu fulani wanaogopaka kama hawataweza kutimiza ahadi yenye wametolea Yehova. Ni kweli kama, wakati fulani unaweza kufanya makosa. Hata wanaume na wanamuke waaminifu wenye Biblia inazungumuzia, walifanyaka makosa. Lakini Yehova haombe watumishi wake wakuwe wakamilifu. (Soma Zaburi 103:13, 14.) Anafurahi wakati unajikaza sana ili kumufurahisha! Atakusaidia. Na hata, anatuhakikishia kama hakuna kitu yenye ‘itaweza kututenganisha na upendo [wake].’​—Soma Waroma 8:38, 39.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone namna kumujua Yehova muzuri na kukubali musaada wake kunaweza kukusaidia kushinda mambo yenye inakuzuia usibatizwe.

4. Ujikaze kumujua Yehova muzuri zaidi

Ni kwa kadiri gani unapaswa kumujua Yehova mbele ubatizwe? Unapaswa kumujua muzuri kabisa, mupaka ufikie kumupenda na kutaka kumufurahisha. Muangalie VIDEO juu muone namna wanafunzi wa Biblia mu dunia yote wamefanya vile. Kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Vile uliona mu video, watu fulani walifanya nini juu ya kujitayarisha kwa ajili ya ubatizo?

Musome Waroma 12:2, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Uko na mashaka juu ya mambo fulani yenye Biblia inafundisha ao ungali najiuliza ikiwa Mashahidi wa Yehova wanafundishaka kweli?

  • Kama ni vile, unaweza kufanya nini?

5. Usiache mambo fulani ikuzuie kubatizwa

Wakati tunaamua kujitoa kwa Yehova na kubatizwa, magumu haikosake. Juu ya kuona mufano, muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Mu hii video, ni mambo gani njo ilikuwa nazuia Narangerel asimutumikie Yehova?

  • Namna gani kumupenda Yehova kulimusaidia ashinde ile mambo?

Musome Mezali 29:25 na 2 Timoteo 1:7, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Nini njo inatupatiaka nguvu ya kushinda mambo yenye inatuzuia kumutumikia Yehova?

6. Yehova atakusaidia

Yehova atakusaidia kufanya mambo yenye inamufurahisha. Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Vile uliona mu video, nini njo ilifanya ule mwanafunzi wa Biblia asiamue kubatizwa?

  • Alijifunza nini yenye ilimusaidia kuwa hakika kama Yehova atamusaidia?

Musome Isaya 41:10, 13, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini unaweza kuwa hakika kama utatimiza ahadi yenye unamutolea Yehova wakati unajitoa kwake?

7. Ukuwe mwenye shukrani sana juu ya upendo wenye Yehova anakuonyesha

Kama unawaza juu ya juu ya mambo mbalimbali yenye inaonyesha kama Yehova anakupenda sana, utakuwa mwenye shukrani zaidi na utatamani sana kumutumikia milele. Musome Zaburi 40:5, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Ni mambo gani yenye Yehova alishakufanyia yenye unafurahia sana?

Yeremia alimupenda Yehova na alipenda neno yake, na aliona kama ni pendeleo kabisa kuitwa kwa jina ya Yehova. Alisema hivi: “Neno lako likakuwa kwangu furaha na shangwe ya moyo wangu, kwa maana jina lako limeitwa juu yangu, Ee Yehova Mungu.” (Yeremia 15:16) Jibia hii maulizo:

  • Juu ya nini ni pendeleo sana kuwa Shahidi wa Yehova?

  • Unapenda kubatizwa juu na weye ukuwe Shahidi wa Yehova?

  • Kuko jambo yenye iko nakuzuia kubatizwa?

  • Unawaza unapaswa kufanya nini juu na weye ufikie kubatizwa?

WATU FULANI WANASEMAKA: “Kama ninabatizwa, sijue kama nitaweza kutimiza ahadi yenye nilitolea Yehova.”

  • Na weye unawazaka vile?

KWA KIFUPI

Yehova anaweza kukusaidia ushinde mambo yenye iko nakuzuia usibatizwe.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Unapaswa kujua Biblia sana mbele ubatizwe?

  • Unaweza kuwa na lazima ya kufanya mabadiliko gani mbele ubatizwe?

  • Juu ya nini haupaswe kuogopa kubatizwa?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona nini njo inapaswa kukuchochea kubatizwa.

“Uko Tayari Kubatizwa?” (Munara wa Mulinzi, Mwezi wa 3, 2020)

Ona namna unaweza kushinda mambo fulani yenye inaweza kukuzuia kubatizwa.

“Ni Kitu Gani Kinanizuia Nisibatizwe?” (Munara wa Mulinzi, Mwezi wa 3, 2019)

Ona namna mwanaume fulani alifikia kushinda mambo yenye ilikuwa namuzuia asibatizwe.

‘Juu ya Nini Unakawia Kubatizwa?’ (1:10)

Ku mwanzo, mwanaume fulani mwenye kuitwa Ataa aliogopa kubatizwa. Ona mambo yenye ilimufanya aamue kubatizwa.

Ninastahili Hizi Baraka Zote? (7:21)